Home »
» TRA Mara yakusanya bil. 79/-
TRA Mara yakusanya bil. 79/-
|
|
WAFANYABIASHARA mkoani Mara, wametakiwa kulipa kodi kwa wakati
kwa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kwa kuzingatia taratibu mbalimbali za
kibiashara ikiwa ni pamoja kuwapatia risiti wateja pindi wanapowauzia
bidhaa.
Wito huo ulitolewa jana na meneja wa TRA mkoani hapa, Joseph Kalinga,
katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mlipa kodi zilizofanyika katika
viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo mjini Musoma.
Aliwataka wafanyabiashara kujijengea mazoea ya kulipa kodi zao kwa
wakati bila udanganyifu ikiwa ni pamoja na kuwasihi kutoa risiti kwa
wateja wao kwa bidhaa wanazokuwa wameuza ili kufanikisha mpango wa
ulipaji kodi.
Awali akisoma taarifa ya makusanyo ya mkoa, Kalinga alisema TRA mkoani
hapa imekusanya zaidi ya sh bilioni 79 kwa mwaka wa fedha 2012/2013
kiasi ambacho ni zaidi ya lengo lililokusudiwa la zaidi ya sh bilioni
68, sawa na asilimia 116.1.
Aidha Kalinga ameongeza kuwa kwa mwaka wa fedha ulioanzia Julai
2013/2014 TRA imekusanya zaidi ya sh bilioni 24, sawa na asilimia 91.24,
huku wakitaraji kukusanya zaidi ya sh bilioni 110.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na
Kilimo (TCCIA) mkoani Mara, Bartazal Bibogo, amezitaja baadhi ya
changamoto zinazoikabili sekta ya uchumi mkoani hapa kuwa ni pamoja na
kufa kwa viwanda, uzalishaji wa chini ya kiwango pamoja na miondombinu
mibovu.
Alisema kama viwanda na miundombinu ikiimarishwa, mamlaka hiyo itaweza kuchangia ukuaji uchumi kwa makusanyo makubwa ya kodi.
Gibogo amevitaja baadhi ya viwanda vilivyokufa na vingine kufanya
chini ya kiwango kuwa ni pamoja na Mutex, Vilian, Musoma Fish Processors
na Prime Ketchi; na kuongeza kuwa serikali na uongozi wa viwanda
wanapaswa kukaa pamoja ili kuangalia chanzo cha kufa au kufanya chini ya
kiwango kwa viwanda hivyo.
Chanzo;Tanzania Daima
|
|
0 comments:
Post a Comment