WANAMABADILIKO WASAIDIA KUPUNGUZA UKATILI WA KIJINSIA WILAYANI TARIME

"Shemeji zangu walikuwa sita walinipiga sana kwa kweli kwa sababu ya kutaka kumiliki Mali za Mume wangu ambaye ni Marehemu" , ni mmoja ya wanawake wa Tarime akisimlia  kwa masikitiko kutokana na ukatili alioupata baada ya kufiwa na mumewe, ambapo ndugu wa mume alilazimisha kumrithi yeye na mali za mumewe. Mila kama hizi zinazomkandamiza mwanamke zinapaswa kusitishwa 
"Tumekubali kabisa watoto wetu wa kike wasiendelee kukeketwa ,lakini bado jamii zetu hazituelewi tunaendelea kuwaelimisha ili nao wabadilike."- Mzee wa Kimila (Aliyesimama). Bado kuna kazi kubwa ya kumaliza swala la ukeketaji lakini kupitia elimu mbalimbali na mafunzo yanayotelewa kuhusu maswala ya ukeketaji juu ya hasara na madhara yake inaendelea kupunguza idadi ya wanaokeketwa.
"Kwa Tarime mwanamke kupigwa na kuvuliwa nguo hadhalani ilikuwa ni kitendo cha kawaida tu" - Sara Boniface (aliyesimama) , alielezea kwa kina kuhusu ukatili wa kupigwa ambapo aliongeza kwamba kwa sasa ukatili huo umepungua kutokana na elimu wanayoipata wanajamii juu ya ukatili wa kijinsia.
Mmoja wa wazee wa Kimira kutoka Tarime(aliyesimama) akieleza juu ya ukeketaji na kudai kuwa mwanamke aliyekeketwa anakuwa na thamani kubwa kama ilivyo kwa mwanamke mweupe kwa wasukuma, hii ni moja ya sababu zinazosababisha ukeketaji uendelee. Ikiwa elimu itaendelea kutolewa ukeketaji huu utapungua kwa kiasi kikubwa.
 "Ukatili wa ukeketaji ulikuwa unafanyika hadharani  kweupe, wazazi walikuwa wanalazimisha mabinti zao kukeketwa ili wapate mahali nyingi zaidi, ambapo fedha hizo ziwasaidie katika kupata kipato zaidi" - Nyakerandi Mariba. Swala hili limepungua sana kutokana na juhudi za wanamabadiliko kuendelea kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia.
"Maswala ya ukatili wa kijinsia yanaleta madhara makubwa katika jamii zetu,hasa kwa mabinti na akina  mama"-Lucy Matemba Afisa maendeleo ya jamii Tarime
Meneja wa kampeni ya Tunaweza Bi. Eunice Mayengela akiendelea kutoa Muongozo wa majadiliano
Wanamabadiliko wakiendelea kufuatilia mjadala
"Kila wiki tunapokea kesi zaidi ya kumi (10) zanazoripotiwa Tarime zikihusu kipigo,ubakaji, ulawiti na wanawake kutishiwa kuuwa,kupigwa sana kisha kubakwa kwa lazima ama kulawitiwa"- Dawati la Jinsia . Licha ya kesi hizo kuwa nyingi lakini elimu inayoendelea kutolewa na kampeni ya tunaweza imesaidia sana kupunguza ukatili wa kijinsia.
Wazee wa Kimila kutoka Tarime wakiteta jambo wakati wa mjadala
 Wanamabadiliko wakiwa katika picha ya pamoja.
Picha na Fredy Njeje

ALIYEMNAJISI MTOTO WAKE HADI KIFO, APEWA SHTAKA LA MAUAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mtoto Mase Denis kutoka Kabwana wilayani Rorya mkoani Mara aliyedaiwa kunajisiwa na baba yake wa kufikia Machi 3, mwaka huu alifariki dunia wakati akiwa njiani kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Rufani Bugando jijini Mwanza juzi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime-Rorya, Henry Mwaibambe aliwaambia waandishi wa habari kuwa awali mtuhumiwa Denis Ondigo alishitakiwa kwa kunajisi lakini kutokana na kifo hicho amebadilishiwa kuwa shtaka la mauaji.

Mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo majira ya saa 6 mchana wa Machi 3 akiwa nyumbani kwake Kabwana  baada ya mama wa mtoto kuwa amekwenda dukani kununua mahitaji ya nyumbani.

Kamanda huyo alisema Ondigo (26) mkazi wa Kabwana alifikishwa Mahakama ya Wilaya Tarime mkoani Mara kwa mara ya kwanza Machi 13.

FASTJET YAWEZESHA MADAKTARI KUSAFIRI KUTOA HUDUMA YA AFYA YA KINYWA NA MENO BURE KWA WANANCHI WILAYANI TARIME

 AQ6A7818.jpg
 Baadhi ya Madaktari watoa huduma ya meno na kimywa  pamoja na  watumishi wa Fastjet wakiwa wamewasili jijini Mwanza wakitokea Dar es salaam.
 AQ6A7930.jpg
 AQ6A7945.jpg
 Madaktari kutoka chama cha madaktari wa kinywa na meno Tanzania wakiwa wilayani tarime mkoa wa mara kuendelea kutoa elimu ya kinywa na meno ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno Duniani, ambapo walikuwa wanatoa huduma za uchunguzi,matibabu na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafikia wanafunzi na watoto yatima.AQ6A7949.jpg
Msemaji wa Fastjet Tanzania Bi. Lucy Mbogoro akiwapatia wanafunzi dawa za mswaki pamoja na miswaki kwa ajili ya kuendelea kuweka meno yao safi pamoja na vinywa vyao.
 AQ6A7959.jpg
Mmoja wa madakrtari wa meno na kinywa akiendelea kutoa elimu kwa wanafunzi.
AQ6A8009.jpg
Mh. Mariam  Mkono, Diwani wa Viti Maalum akizungumza na madaktari wa kinywa na meno kijijini Nyamwaga. 
 AQ6A8014.jpg
Debora Magasi, Muuguzi Mkuu wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya akizungumza na madaktari wa kinywa na meno kijijini Nyamwaga
AQ6A8020.jpg
Mganga Mkuu wa Kinywa na Meno wa Mkoawa Mara, Dkt Nila Jackson, alisema kati ya Machi 13 hadi 16 mwaka huu madaktari hao walifikia jumla ya wananchi 710  katika kijiji cha Nyamwaga wakiwemo wanafunzi 510 kutoka shule za msingi saba kijijini humo.
AQ6A8024.jpg

Raiswa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania Dkt. Ambege Jack Mwakatobe, alitoa wito kwa madaktari wa mikoa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi angalau mara mbili kwa mwezi ili kuwaongezea ufahamu na uelewa wananchi juu yausafi wa kinywa.

***********
SHIRIKA la Ndege la Fastjet limewezesha Madaktari wa kinywa na meno kusafiri kwenda kutoa huduma ya afya ya kinywa na meno bure kwa wananchi wa wilaya ni Tarime mkoani Mara.



Madaktari kutokachama cha madaktari wa kinywa na meno Tanzania wameanza ziara ya kujitolea katika wilaya ya Tarime mkoani mara ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno duniani ambapo watatoa huduma zauchunguzi, matibabu na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafikia wanafunzi na watoto yatima.



Akizungumza hivi karibuni wilayani Tarime, Daktari wa Meno wa Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Dk. David Mapunda, alisema ziara hiyo itawapatia fursa madaktari hao kufanya uchunguzi wa kinywa pamoja na kutoa huduma za matibabu pamoja na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Alisema miongoni mwa magonjwa yanayosumbua katika kinywa ni pamoja nakuoza kwa meno na ugonjwa wa fizi ambayo yanasababishwa na uchafu unaotokana na kutokupiga mswaki, kukosea kupiga mswaki au kutumia mswakiusio faa.

Alisema ili wananchi waepukane na magonjwa hayo ya meno wanapaswa kupiga mswaki angalau mara mbili kwa siku na kujenga utaratibu wa kuangalia afya ya kinywa na meno mara kwa mara.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Kinywa na Meno wa Mkoawa Mara, Dkt Nila Jackson, alisema kati ya Machi13 hadi 16 mwaka huu madaktari hao walifikia jumla ya wananchi 710 katika kijiji cha Nyamwaga wakiwemo wanafunzi 510 kutoka shule zamsingi saba kijijini humo.

"Kati ya tarehe hizo Madaktari hao  walitoa uchunguzi, matibabu na elimu ya afya ya kinywa na meno na kati ya tarehe 17 hadi 20 watakuwa katika wilaya ya Tarime na Rorya kuendelea na zoezi hilo," aliongeza Dk.Jackson

Naye Raiswa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania (Tanzania Dental Association), Dkt. Ambege Jack Mwakatobe, alitaja kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya kinywa na meno Duniani inayosema “Sema ah, fikiri akinywa, fikiria afya” ambayo inalenga kuwahamasisha wananchi kuzingatia afya ya kinywa na meno ilikujikinga na magonjwa yanayohusiana na ugonjwa wa meno ikiwemo magonjwa yakisukari na mengine.

Aidha alitoa wito kwa madaktari wa mikoa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi angalau mara mbili kwa mwezi ili kuwaongezea ufahamu na uelewa wananchi juu ya usafi wa kinywa.

Akizungumza kutoka kijiji cha Nyamwaga, Msemaji wafastjet nchini, Lucy Mbogoro,  alisema shirika la fastjet linafuraha kuwa sehemu ya shughuli hii inayofanywa na madaktari hawa wazalendo.

"Shirika la fastjet limewawezesha madaktari hawa kusafirikutoka Dar es salaam hadi Mwanza na kurudi ikiwa ni sehemu yampango wake wakurudisha shukrani kwajamii," alisema.

 

PROF. MBARAWA ATOA MIEZI 9 KWA MKANDARASI NYAZA ROADS WORKS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kisorya, wilaya ya Bunda alipokutana nao baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 inayojengwa kwa kiwango cha lami, wilayani humo, mkoani Mara.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, akisisitiza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, katika ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 inayojengwa kwa kiwango cha lami, wilayani Bunda, mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Kangi Lugola, ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mwibara, akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, wakati wa ukaguzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 inayojengwa kwa kiwango cha lami, wilayani Bunda, mkoani Mara.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 inayojengwa kwa kiwango cha lami, wilayani Bunda, mkoani Mara.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Makutano-Sanzate yenye urefu wa KM 50 inayojengwa kwa kiwango cha lami ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 54. Barabara hiyo inajengwa na wakandarasi wazawa M/S Mbutu JV.

…………………

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemtaka mkandarasi Nyanza Road Works kukamilisha ujenzi wa barabara ya Bulamba-Kisorya yenye urefu wa KM 51 kwa kiwango cha lami ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.

Prof. Mbarawa ametoa kauli hiyo wakati akikagua ujenzi wa barabara hiyo na kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Kisorya na kusema kuwa usanifu wa barabara na madaraja katika barabara hiyo umewasilishwa sasa ni jukumu la mkandarasi kuendelea na ujenzi kwa kasi na kwa viwango vya ubora.

“Serikali ina nia njema kwa wananchi wa wilaya ya Bunda na mkoa wa Mara sasa tunaijenga barabara hii na mwishon mwa mwaka mtaanza kunufaika nayo”, amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo utarahisisha mawasiliano na kupunguza gharama za shughuli za usafirishaji wa samaki, mazao na abiria, uboreshaji makazi na kukuza uchumi kwa maeneo yaliyo kando ya barabara.

Kuhusu suala la fidia, Prof. Mbarawa amefafanua kuwa Serikali italipa fidia kwa mwananchi ambaye barabara imemfuata kama anavyostahili.

“Serikali haina nia ya kumuonea mtu yeyote bali inachofanya inalipa kulingana na sheria inavyoelekeza”, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Katika hatua nyingine Waziri Prof. Mbarawa amekagua ujenzi wa barabara ya Makutano-Sanzale KM 50 na kumwagiza mkandarasi wa M/S Mbutu JV Contractor (T) kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kabla ya mwezi Julai mwaka huu.

“Mradi huu ni wa muda mrefu sana na wananchi wameusubiri kwa muda kama hamtamaliza mradi huu mpaka mwezi juni, hii itakuwa kazi yenu ya mwisho, maana ninategemea nyinyi kama wazawa mngekuwa wa mfano” amesisitiza Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima amesema kwa sasa mkoa umeamua kupata taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa miradi ya barabara kila baada ya miezi mitatu ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Mara, Mhandisi Mlima Ngaile amesema Wakala utasimamia mradi wa ujenzi wa barabara hizo na kuhakikisha mradi unazingatia viwango kulingana na mkataba.

Waziri Prof. Mbarawa yuko mkoani Mara kwa ziara ya siku mbili akiwa na lengo la kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya sekta ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano.

Kamishna wa TRA amsimamisha kazi Meneja wa Mara

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),  Charles Kichere amemsimamisha kazi Meneja wa TRA Mkoa wa Mara  Nicodemus Mwakilembe kwa kushindwa kusimamia vizuri mashine za  Kielektroniki za Kutolea Risiti (EFDs).

Uamuzi huo umetokana na ziara ya kushtukiza ya kukagua matumizi ya EFD aliyoifanya Kamshina Mkuu wa Tra kwenye baadhi ya maduka ya biashara Wilayani Bunda Mkoa wa Mara.

Akizungumza mara baada ya ziara yake, Kamishna Mkuu Kichere alisema kuna wafanyabishara wengi mkoani Mara  ambao walishalipa fedha kwa ajili ya kupata mashine za EFD lakini mpaka sasa hawajapatiwa mashine hizo.

"Katika ziara yangu nimegundua kwamba, wapo wafanyabiashara ambao wameshalipia mashine tangu mwaka 2013, 2014 na 2015 lakini mpaka sasa bado hawajapatiwa mashine za EFD na wamekuwa wakitumia mwanya huo kama kinga ya kutochukuliwa adhabu na TRA wakati Meneja wa Mkoa  yupo na hachukui hatua zozote. Huu ni uzembe uliopitiliza na kamwe siwezi kuuvumilia," amesema  Kichere.


Kichere amewaagiza mameneja wote wa TRA nchi nzima pamoja na majukumu mengine, kuhakikisha wanasimamia kikamilifu matumizi ya mashine za EFD katika mikoa yao na amesema hatasita kumuwajibisha meneja yeyote atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Ziara hiyo ya kushtukiza imewawezesha wafanyabiashara waliokuwa wamelipia mashine za EFD miaka ya nyuma, kupata mashine hizo na kufundishwa jinsi ya kuzitumia ambapo wengine wamejitokeza kununua mashine hizo kwa ajili ya biashara zao.

Kamishna  Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania yuko mkoani Mara kwa ziara ya siku tano  ambapo amepata nafasi ya kutembelea Vituo vya Forodha mipakani na ofisi mbalimbali za mamlaka hiyo pamoja na baadhi ya wafanyabiashara akikagua matumizi ya mashine za EFD.

KAMISHNA MKUU WA TRA AMSIMAMISHA KAZI MENEJA WA TRA MKOA WA MARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (aliyekaa mbele) akiongea na kutoa maagizo kwa Meneja wa TRA Wilaya ya Bunda Mkoani Mara pamoja na wafanyakazi wengine wa Mamlaka hiyo kuhusu ukusanyaji wa mapato ya Serikali mara alipotembelea ofisi ya TRA Wilayani hapo ili kujionea namna ukusanyaji mapato unavyofanyika mapema 3 Februari, 2018.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akimsisitizia jambo Mfanyabiashara wa duka la nguo Wilayani Bunda Mkoani Mara kuhusu suala la umuhimu wa kutumia mashine ya Kielektroniki ya Kutolea Risiti (EFD) mara alipofanya ukaguzi wa mashine hizo katika baadhi ya maduka Wilayani hapo 3 Februari, 2018.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akikagua taarifa ya mauzo ya siku ya Mashine ya Kielektroniki ya Kutolea Risiti (EFD) toka kwa Wafanyabiashara wa duka la vifaa vya nyumbani Wilayani Bunda Mkoani Mara mara alipofanya ukaguzi wa mashine hizo katika baadhi ya maduka Wilayani hapo 3 Februari, 2018.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa TRA Wilaya ya Bunda Mkoani Mara pamoja na wafanyakazi wengine wa Mamlaka hiyo mara alipotembelea ofisi ya TRA Wilayani hapo ili kujionea namna ukusanyaji mapato unavyofanyika mapema 3 Februari, 2018.(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-TRA).



Na: Veronica Kazimoto-Bunda, 

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere amemsimamisha kazi Meneja wa TRA Mkoa wa Mara Ndg. Nicodemus Mwakilembe kutokana na uzembe wa kutosimamia vizuri matumizi ya Mashine za Kielektroniki za Kutolea Risiti (EFDs) kwa wafanyabiashara wa mkoani kwake. 

Uamuzi huo umetokana na ziara ya kushtukiza ya kukagua matumizi ya EFD aliyoifanya Kamshina Mkuu wa TRA kwenye baadhi ya maduka ya biashara Wilayani Bunda Mkoa wa Mara. Akizungumza mara baada ya ziara yake, Kamishna Mkuu Kichere alisema Meneja huyo ameonyesha uzembe wa hali ya juu kwani kuna wafanyabishara wengi mkoani kwake ambao walishalipa fedha kwa ajili ya kupata mashine za EFD lakini mpaka sasa hawajapatiwa mashine hizo. 

"Katika ziara yangu nimegundua kwamba, wapo wafanyabiashara ambao walikwisha kulipia mashine tangu mwaka 2013, 2014 na 2015 lakini mpaka sasa bado hawajapatiwa mashine za EFD na wamekuwa wakitumia mwanya huo kama kinga ya kutochukuliwa adhabu na TRA wakati Meneja wa Mkoa yupo na hachukui hatua zozote. Huu ni uzembe uliopitiliza na kamwe siwezi kuuvumilia," alisema Kichere. 

Kutokana na uzembe huo, Kamishna Mkuu Kichere amewaagiza Mameneja wote wa TRA nchi nzima pamoja na majukumu mengine, kuhakikisha wanasimamia kikamilifu matumizi ya mashine za EFD katika mikoa yao na amesema hatasita kumuwajibisha Meneja yeyote atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo. 

Ziara hiyo ya kushtukiza imewawezesha wafanyabiashara waliokuwa wamelipia mashine za EFD miaka ya nyuma, kupata mashine hizo na kufundishwa jinsi ya kuzitumia ambapo wengine wamejitokeza kununua mashine hizo kwa ajili ya biashara zao. Kamishna Mkuu aliongeza kuwa, mashine za EFD zina umuhimu sio tu kwa Serikali kupata mapato bali kwa wafanyabiashara husika kwani huwawezesha kutunza kumbukumbu, kujua mwenendo halisi wa biashara zao na hatimaye kulipa kodi stahiki. 

Sambamba na hayo, Kichere amewataka wananchi wasiishie tu kudai risiti bali wakishachukua risiti hizo wazikague ili kuthibitisha uhalali wake na usahihi wa kiasi cha pesa walicholipa. Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania yuko mkoani Mara kwa ziara ya siku 5 ambapo amepata nafasi ya kutembelea Vituo vya Forodha mipakani na ofisi mbalimbali za mamlaka hiyo pamoja na baadhi ya wafanyabiashara akikagua matumizi ya mashine za EFD.

SHIRIKA LA AGPAHI YAKABIDHI KOMPYUTA 46 KWA AJILI YA VITUO VYA TIBA NA MATUNZO KWA WATU WANAOISHI NA VVU MKOA WA MARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limekabidhi kompyuta 46 zenye thamani ya shilingi milioni 70.2 zitakazotumika katika vituo vya tiba na matunzo (CTC) kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) kwenye halmashauri za wilaya mkoani Mara.
Shirika hilo limekabidhi kompyuta hizo siku ya Jumatatu, Januari 22, 2018 kwa Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Nyanda katika ukumbi wa mikutano wa Mwembeni uliopo katika Manispaa ya Musoma.
Akizungumza wakati wa kukabidhi kompyuta hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa alisema kompyuta hizo zitatumika kuhifadhi takwimu za wateja katika vituo vya tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU na kusaidia upatikanaji wa taarifa kwa haraka na kwa usahihi zaidi.

“Leo tunayo furaha kukabidhi kompyuta 19 ambayo ni nyongeza ya kompyuta 27 ambazo zimeshapelekwa kwenye vituo vya afya hivyo hadi sasa tutakuwa tumekabidhi jumla ya kompyuta 46 tulizokabidhi kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu tuanze kutekeleza miradi ya Ukimwi katika mkoa wa Mara”, alieleza Dk. Sekela.
“Mbali na kukabidhi kompyuta pia tumefanikisha ajira kwa makarani takwimu "Data Clerks" 84 kwa halmashauri zote na tunawezesha upatikanaji wa mtandao wa intaneti kwa kutoa modem ili kurahisisha uingizaji wa takwimu katika mfumo wa kielektroniki na kutoa taarifa kwa wakati stahiki”,aliongeza Dk. Sekela.
Katika hatua nyingine alisema shirika hilo linatekeleza miradi ya Ukimwi katika vituo 112 vya kutolea huduma za afya mkoani Mara, kati ya vituo hivyo 67 ni vituo vya kutolea tiba na matunzo na 46 ni vya kutolea huduma ya kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).
Dk. Sekela alibainisha kuwa katika kipindi cha mwezi Oktoba 2016 hadi Septemba 2017, jumla ya watu 182,712 mkoani humo walipata huduma ya upimaji wa VVU, kati yao wanaume walikuwa 51,868 (28%), watoto 31,423 (17%). Kati ya watu 182,712 waliopima, 7,325 (4%) waligundulika kuwa na maambuzi ya VVU na 6,022 (82%) walianzishiwa dawa za kupunguza makali ya VVU. 
Aliongeza kuwa katika kipindi hicho pia akina mama wajawazito 49,937 walipima VVU , kati yao 981 sawa na 2% waligundulika kuwa na maambukizi ya VVU na 755 sawa na 77% walianzishiwa dawa za kupunguza makali ya VVU.
Akipokea kompyuta hizo, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Nyanda alilishukuru shirika la AGPAHI kwa kutoa msaada huo na kuzitaka halmashauri za wilaya kuzitunza ili zidumu.

“Tunawashukuru sana AGPAHI na Watu wa Marekani kwa kuendelea kutushika mkono katika sekta afya, mwaka huu mmetuongeza shilingi bilioni 7.2 kwenye bajeti ya mkoa kwa ajili ya masuala ya Ukimwi, kwa kweli mmekuwa wadau wakubwa wa afya, naomba tuendelee kushirikiana kuwahudumia wananchi”, alieleza Nyanda.

“Serikali ya mkoa itasimamia vizuri fedha hizi,wakurugenzi tumieni fedha za wafadhili kwa malengo yaliyokusudiwa, msihamishe fedha, pia tuache tabia ya kufanya kazi kwa mazoea na watendaji hakikisheni mnatoa takwimu sahihi", alisema Nyanda.
Mbali na kukabidhi kompyuta, Shirika la AGPAHI pia linaendesha mafunzo ya siku mbili kuhusu taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za wafadhili ambao ni Watu wa Marekani kupitia Centres for Disease Control (CDC) yaliyohudhuriwa na wakurugenzi na viongozi wa timu za afya za mikoa na wilaya.
Wakurugenzi wa halmashauri za wilaya wanaojengewa uwezo ni kutoka Mji wa Bunda,Tarime Mji, Manispaa ya Musoma, Bunda Vijijini, Butiama, Musoma Vijijini, Rorya,Tarime na Serengeti na timu za afya za mkoa na wilaya kuhusu namna ya kutumia fedha za mfadhili sawa sawa na matakwa na makubaliano kati ya AGPAHI na serikali ya Marekani.
Mwaka huu shirika limetoa shilingi bilioni 7.2 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Ukimwi mkoani Mara ikiwa ni mara sita zaidi ya fedha iliyotolewa na shirika hilo mwaka 2016/2017 ambayo ilikuwa shilingi bilioni 1.1.
Shirika la AGPAHI linatekeleza miradi ya Ukimwi katika mikoa sita nchini ambayo ni Shinyanga, Simiyu, Geita,Mwanza, Tanga na Mara likishirikiana na serikali ya Tanzania kwa ufadhili wa serikali ya Watu wa Marekani kupitia CDC katika kutekeleza mradi wa “Boresha” ambao unatoa huduma za kinga, tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU na Ukimwi.


Mgeni rasmi, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Nyanda akizungumza wakati wa zoezi la makabidhiano ya kompyuta na kufungua mafunzo ya taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za wafadhili katika ukumbi wa mikutano wa Mwembeni manispaa ya Musoma.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Nyanda akilishukuru shirika la AGPAHI kwa kuipatia serikali ya mkoa wa Mara shilingi bilioni 7.2 kwa ajili ya miradi ya Ukimwi.
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa akizungumza wakati wa kukabidhi kompyuta 46. Kushoto ni Meneja wa Shirika la AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dk. Nkingwa Mabelele. Kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Raphael Nyanda.
Dk. Sekela alisema kompyuta hizo zitatumika kuhifadhi takwimu za wateja wa CTC katika vituo vya afya na kusaidia upatikanaji wa taarifa kwa haraka na kwa usahihi zaidi.
Dk. Sekela akizungumza wakati wa kukabidhi kompyuta hizo.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Mara, Dk. Francis Mwanisi akilishukuru shirika la AGPAHI kwa msaada wa kompyuta 46.
Maboksi yenye kompyuta zilizotolewa na shirika la AGPAHI kabla ya kukabidhiwa kwa wakurugenzi wa halmashauri za wilaya mkoani Mara.
Katikati ni Dk. Sekela akionyesha moja kati ya kompyuta 46 zilizotolewa na shirika la AGPAHI. 
Dk. Sekela akielezea zaidi kuhusu kompyuta hizo.
Dk. Sekela na Kaimu Katibu Tawala, Raphael Nyanda wakikabidhi kompyuta kwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Rorya Charles Kitamuru Chacha (aliyevaa nguo nyeusi kushoto) aliyeambatana na timu ya afya ya halmashauri hiyo.
Makabidhiano kwa viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Butiama yakiendelea.
Viongozi wa halmashauri ya Manispaa ya Musoma wakiongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Fidelica Myovela (aliyeshika boksi la kompyuta) wakipokea kompyuta.
Zoezi la makabidhiano ya kompyuta likiendelea.
Viongozi wa timu za afya za mikoa na wilaya wakiwa ukumbini.
Mratibu wa AGPAHI mkoa wa Mara, Alio Hussein akielezea lengo la mafunzo ya taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za wafadhili ambao ni Watu wa Marekani kupitia Centres for Disease Control (CDC).
Alio Hussein alisema shirika hilo linatekeleza miradi ya Ukimwi kwenye halmashauri 9 za wilaya mkoani Mara.
Afisa Ruzuku Mwandamizi wa shirika la AGPAHI, Leticia Gilba akitoa mada kuhusu vigezo na masharti ya mkataba wa utekelezaji wa Mradi wa Boresha mkoani Mara unaofadhiliwa na Watu wa Marekani kupitia CDC.
Leticia Gilba akiendelea kutoa mada ukumbini. 
Leticia Gilba akielezea kuhusu sheria na taratibu za matumizi ya fedha za wafadhili.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Rorya, Charles Kitamuru Chacha akichangia mada wakati wa mafunzo hayo.
Mratibu wa Ukimwi wa halmashauri ya wilaya ya Musoma, Mwanaidi Francis akichangia hoja wakati wa majadiliano ukumbini.
Kaimu Mganga Mfawidhi hospitali teule ya wilaya ya Rorya, Dk. Baraka Malegesi akichangia hoja wakati wa mafunzo hayo.
Picha ya pamoja - wafanyakazi wa AGPAHI, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na timu za afya za mkoa na wilaya. 
Picha ya pamoja.
 
CREDIT:MALUNDE BLOG

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa