VIONGOZI WA TAASISI, NA WAHALMASHAURI ZOTE MBILI WATETA NA MKUU WA WILAYA.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge siku ya tarehe 25/3/2025 amefanya kikao kazi na viongozi wa Halmashauri zote mbili pamoja na wa taasisi za serikali zilizopo katika Wilaya ya Bunda.

Mh.Kaminyoge alisema lengo kuu la kikao hiki ni kujitambulisha kwenu nikiwa ndiye Mkuu wa Wilaya hii baada ya mabadiliko yaliyofanywa na Mh. Rais siku chache zilizopita, na pia kuwatambua nyie viongozi wote mliopo mahali hapa, pamoja na kuomba ushirikiano wenu ili tuweze kufanya kazi kwa pamoja na ushirikiano katika kuhakikisha tunawaletea wananchi wa Wilaya hii maendeleo na kuhakikisha wanaishi kwa amani, furaha na usalama.

Katika kikao hicho viongozi kutoka ngazi ya vijiji, kata na mitaa wote walihudhuria, ambapo walimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuwaalika katika kikao hicho na kumuahidi kumpa ushirikiano wote katika kuhakikisha wanawaletea maendeleo wananchi wa Bunda katika katika sekta zote za elimu, Afya, maji, nishati na miundombinu iliyobora na mizuri katika kuhakikisha wanaleta na kukuza maendeleo ya wanaBunda.

Mh. Kaminyoge aliweza kusikiliza kero na changamoto ambazo viongozi hao wamekuwa wakizipitia katika utendaji wao wa kazi, ambapo kupitia wakuu wa idara na vitengo waliweza kuzitatua na kuwafafanulia kulingana na Sheria kanuni na taratibu za kazi.

Mkuu wa Wilaya aliwaomba viongozi hao kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja na kuhakikisha Kila mtu anatimiza majukumu yake ya KAZI kwa kufuata kanuni, taratibu na Sheria za kazi, na pale wanapohitaji kuonana nae milango ya ofisi yake IPO wazi na Kila mtu anaruhusiwa kuja kuongea nae pale anapohitaji ufafanuzi au ushirikishwaji wake kama Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mh. Kaminyoge aliwaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa idara na vitengo kuhakikisha wanaandaa miradi ambayo itatembelewa na mwenge wa uhuru, 2025 wakishirikiana na taasisi katika kuhakikisha maandalizi ya mapokezi ya mwenge yanaanza mapema kwa kubainisha miradi yote na njia 










KUTOKA BUNDA: WENYEVITI WA VIJIJI NA MTAA MARUFUKU KUMILIKI MUHURI.

Katika kikao cha mkutano wa Halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bunda kilichofanyika siku ya tarehe 20/3/2025 katika ukumbi wa Malaika, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge alisoma waraka wenye muongozo unaokataza wenyeviti wa vijiji na mitaa kumiliki muhuri.

Lengo la kusoma waraka huo ni baada ya wenyeviti wa vijiji na mitaa kuomba kumiliki muhuri hiyo kama kitendea kazi chao, kitu ambacho Mkuu wa Wilaya ilibidi kusoma waraka huo ambao umeelezea na kutolea ufafanuzi kwanini hawapaswi kuwa nao na vifaa ambavyo wanatakiwa kuwa navyo kama sehemu ya vitendea kazi.

Mh.Kaminyoge alisema wajibu wa mwenyekiti wa MTAA na Kijiji ni kusimamia, kuhamasisha, kufuatilia, kuongoza, kuwasilisha, kushirikisha, kusuluhisha, kuhifadhi na kudumisha amani katika MTAA au kijiji anachoongoza. 

Muongozo wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali mitaa wenye kumb. Na. CCB.126/215/01 wa tarehe 30/11/2016 unaelezea matumizi ya mihuri kwa wenyeviti wa mitaa na vijiji kwamba wanatakiwa kuacha mara Moja kutumia mihuri katika majukumu ya kiutendaji na badala yake uwekaji au ugongaji wa mihuri ufanywe na maafisa watendaji wa eneo husika.

Pale ambapo MTAA au kijiji hakuna Mtendaji wa MTAA au kijiji, mwenyekiti wa MTAA au kijiji amtambulishe Mwananchi mwenye kuhitaji huduma ya kugongewa muhuri kwa Mtendaji wa kata ili aweze kugongewa muhuri wa kata.

Hivyo basi, kwa mujibu wa taratibu za kazi za mwenyekiti wa MTAA na Kijiji aliyechaguliwa na wananchi anatakiwa kuwa au kumiliki vifaa vifuatavyo ambavyo ni bendera yenye nembo ya Halmashauri, rejista ya wakazi wa MTAA au kijiji na daftari la mihtasari ya vikao vya MTAA au kijiji.

Mh. Kaminyoge aliwaagiza Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia utekelezaji wa maelekezo haya ili kuweza kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima katika mitaa na vijiji.

" Watendaji wa mitaa na vijiji watakaobainika kutumia mihuri vibaya na kuendeleza migogoro hususani ya ardhi watachukuliwa hatua Kali za kisheria." Alisema Mkuu wa Wilaya.





ASANTENI NA KWAHERINI HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru, 2024 ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava siku ya tarehe 3/8/2024 aliwashukuru Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa mapokezi mazuri waliyoyapata.

Ndugu Mnzava alikiri kupokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney kuhusiana na mkesha wa Mbio za Mwenge, na shughuli zote zilizofanyika wakati wa mkesha.

Pia, alishauri wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuhakikisha wanapima afya zao mara kwa mara na kuwa na mazoea ya kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao.

TUNZA MAZINGIRA NA SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA TAIFA ENDELEVU.


MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney siku ya tarehe 2/8/2024 akipokea Mwenge wa uhuru katika viwanja vya shule ya msingi Nyamuswa B, kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Mh. Moses Kaigele.

Mh Dkt Anney amesema Mwenge wa uhuru utakimbizwa km 109 na utatembelea, kukagua na kuzindua miradi nane ya maendeleo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, yenye thamani ya Tshs bilioni 2,312,165,470.

 

MWENGE WA UHURU, 2024 WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALAMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Mwenge wa uhuru, 2024 umezindua miradi minne ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, siku ya tarehe 2/8/2024.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava amezindua mradi wa huduma za jamii, ambayo ni nyumba ya kulala wageni yenye thamani ya Tshs million 230 iliyopo Nyamuswa.

Pia, alizindua nyumba ya watumishi (3in1), iliyopo Kata ya Hunyari katika kituo cha Afya Hunyari na shule ya Sekondari ya Mariwanda, na mradi wa maji Sanzante.

Ndugu Mnzava alisisitiza wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuhakikisha wanashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha wanaenda kupiga kura ili waweze kuchangua viongozi Bora, na aliwasisistiza kuhakikisha wanatunza mazingira kwa kuhakikisha kila kaya inapanda Miti mitano.

Mbio za Mwenge wa uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, imetembelea, kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo.

 

MOTISHA YATOLEWA KWA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI, KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA



Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney ametoa ngao za motisha kwa Wakuu wa shule za Sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mh. Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi

Mhe. Mtambi alizitaka shule ambazo zimefanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha Nne mwaka 2023 kuhakikisha wanapewa ngao yenye kuwaongezea motisha zaidi ili waweze kuongeza juhudi katika ufundishaji wa watoto shuleni, na kwa zile shule ambazo hazikufanya vizuri pia, wakuu wa shule wapewe vinyago ambavyo wataviweka katika ofisi zao ili kuongeza motisha ya ufundishaji katika shule.

Kupitia hafla hiyo iliyofanyika tarehe 15 July 2024 ukumbi wa halmashauri ya mji wa Bunda, Mkuu wa Wilaya ya Bunda aliikabidhi shule ya sekondari Ikizu ngao ya ushindi na kutoa kinyago kwa sekondari Hunyari kwa kuburuza mkia kwa shule za halmashauri ya wilaya.

Akikabidhi tuzo hizo, Mhe. Anney alimshukuru Mh Mkuu wa mkoa wa Mara kwa kuwa na upendo kwa Walimu na kupendekeza wazo hilo litakalosaidia kuinua kiwango cha ufaulu

"Hii ilikuwa ni ajenda yangu ya kwanza tangu nilipofika katika Wilaya hii ya Bunda, Elimu ni fursa, Elimu ni chombo cha ukombozi na Elimu inamfanya mtu kuishi na kwenda eneo lolote Duniani, leo hii tupo hapa kwa ajili ya kutoa motisha chanya kwa shule zilizofanya vizuri kwa kutoa ngao ya pongezi na shule zilizofanya vibaya pia tutawapa kinyago ili kuongeza motisha zaidi katika ufundishaji wa watoto shuleni." Alisema

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Ndugu George S Mbilinyi alisema Halmashauri ya Wilaya ya Bunda inajumla ya shule za Sekondari 26, mbili zikiwa ni za binafsi na 24 za serikali.

" Tunampongeza Mhe. Mkuu wa Wilaya kwa kuweza kutimiza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Mara la kuwataka tuwapatie motisha hizi wakuu wa shule za sekondari kwa waliofanya vizuri na waliofanya vibaya katika matokeo ya kidato cha Nne 2023". Alisema Mbilinyi

Naye Kaimu Afisa Elimu Sekondari Bi. Nambua Semlugu amesema "tunatakiwa tusimamie vizuri suala la lishe na utoro shuleni, hii itapunguza idadi ya wanafunzi shuleni kufeli na itaongeza umakini zaidi darasani.

" Binafsi tukio hili linatarajia kuleta matokeo mazuri katika shule zetu, kwa niaba ya Walimu tunaahidi kuwajibika kwa kuhakikisha tunaongeza juhudi zaidi, ombi langu ni kwamba, vinyago vinavyoletwa katika shule zilizofanya vibaya, visiwe vya Wakuu wa shule pekee ama shule pekee bali, viwe vya jamii nzima." Alisema Majura.



RC MTAMBI, WANAHABARI NA WADAU WA MAENDELEO WALIVYOBEBA MDAHALO WA MARA BORA KWA UWEKEZAJI NA KUISHI



Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi (katikati) akizungumza katika Mdahalo wa Mara Bora kwa Uwekezaji na Kuishi, mjini Musoma.  Wanaomsikiliza kwa makini ni Mwenyekiti wa MRPC, Mugini Jacob (wa pili kushoto), Katibu wa MRPC, Pendo Mwakyembe (kushoto), Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Mjanakheri Ibrahim (kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo sehemu ya Viwanda na Biashara, Gambaless Timotheo (wa pili kulia).
------------------------------------------------------

Na Christopher Gamaina, Musoma
----------------------------------------------

Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, waandishi wa habari na wadau mbalimbali wa maendeleo wamejadili fursa za uwekezaji zilizopo mkoani humo na kutaka msukumo wa kuzitangaza uongezwe ili zifahamike kwa watu wengi ndani na nje ya Tanzania.

Hatua hiyo ilifikiwa katika Mdahalo wa Mara Bora kwa Uwekezaji na Kuishi, ulioandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara (MRPC), na kufanyika kwenye Hoteli ya MK mjini Musoma jana

Fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Mara zilizotajwa na kujadiliwa katika mdahalo huo uliofana kwa aina yake, ni pamoja na ufugaji, uvuvi, uchimbaji madini, utalii na kilimo cha mazao ya biashara na chakula.
Sehemu ya waandishi wa habari walioshiriki mdahalo huo.
--------------------------------------------------

Katika hotuba yake, mgeni rasmi RC Mtambi alisema mkoa wa Mara una utajiri wa maliasili na rasilimali nyingi, lakini hazijatangazwa ipasavyo ili kuwashawishi watu wengi kujitokeza kuwekeza kwenye biashara zinazohusiana nazo.

Maliasili na rasilimali hizo ni pamoja na Hifadhi ya Taifa Serengeti, Ziwa Victoria, madini aina ya dhahabu, mifugo na ardhi kubwa inayofaa kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara - kama vile mahindi, ndizi, kahawa, pamba, alizeti na viazi vitamu.

“Lakini pia, tuna miradi mikubwa iliyojengwa na inayoendelea kutekelezwa na serikali; tuna Uwanja wa Ndege Musoma, Hospitali ya Rufaa Kwangwa, Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere kule Butiama, na barabara zinaendelea kuboreshwa katika mkoa mzima.

“Neema hii tuliyo nayo katika mkoa wa Mara haijatangazwa vizuri. Ninawaomba waandishi wa habari mtumie kalamu zenu kutangaza fursa hizi kwa maendeleo ya mkoa wetu na Taifa kwa ujumla,” alisema RC Mtambi.

Kiongozi huyo wa mkoa alitumia nafasi hiyo pia kuipongeza MRPC kwa kuandaa mdahalo huo na kuanzisha mpango wa tuzo za kila mwaka kwa waandishi wa habari wa mkoani Mara watakaokuwa wanafanya vizuri.
Waandishi wa habari wakifuatilia mada katika mdahalo huo.
-----------------------------------------------

Awali, Mwenyekiti wa MRPC, Mugini Jacob alimshukuru RC Mtambi kwa kukubali kuwa mgeni rasmi, pamoja na wadau wa maendeleo walioitikia wito wa kushiriki mdahalo huo.


Tuzo kwa waandishi

Kuhusu tuzo kwa waandishi wa habari - zitakazojulikana kwa jina la Mara Quality Journalism Awards, Jacob alisema zitaanza kutolewa Desemba mwaka huu na kwamba washindi watazawadiwa vyeti na fedha taslimu.

“Tuzo hizi zitakuwa sehemu ya juhudi za kuhamasisha uandishi bora (promoting quality journalism), ambao pia unachangia kuufanya mkoa wa Mara kuwa sehemu bora kwa uwekezaji na kuishi.


Alitaja makundi ya habari zitakazohusika katika tuzo hizo kuwa ni kilimo, ufugaji, madini, utalii, ujenzi na miundombinu, uhifadhi wa wanyamapori, maji, uvuvi endelevelu (sustainable fishing) na makundi maalum ya jamii.


“Tunaamini uandishi bora, yaani quality journalism katika maeneo hayo utasaidia kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongoza na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Mara na Taifa letu la Tanzania kwa ujumla,” alisema Jacob.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo wa MRPC (kushoto) alimkabidhi RC Mtambi zawadi ya kumkaribisha mkoani Mara, yenye picha yake na fursa za uwekezaji zinazopatikana mkoani humo, iliyoandaliwa na klabu hiyo.


Mbali na waandishi wa habari, baadhi ya wadau wa maendeleo wa mkoani Mara walioshiriki katika mdahalo huo ni kutoka Mgodi wa Barrick North Mara, Grumeti Reserves/ Grumeti Fund, HAIPPA PLC, Nyihita Sunflower, CCM, TANROADS, TCCIA, WAMACU, Kampuni ya Swala na Benki ya Azania, miongoni mwa wengine.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, viongozi wa MRPC na wadau mbalimbali wa maendeleo (wa nne kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuhitimisha mdahalo huo. (Picha zote na Mara Online News)

WANAMABADILIKO WASAIDIA KUPUNGUZA UKATILI WA KIJINSIA WILAYANI TARIME

"Shemeji zangu walikuwa sita walinipiga sana kwa kweli kwa sababu ya kutaka kumiliki Mali za Mume wangu ambaye ni Marehemu" , ni mmoja ya wanawake wa Tarime akisimlia  kwa masikitiko kutokana na ukatili alioupata baada ya kufiwa na mumewe, ambapo ndugu wa mume alilazimisha kumrithi yeye na mali za mumewe. Mila kama hizi zinazomkandamiza mwanamke zinapaswa kusitishwa 
"Tumekubali kabisa watoto wetu wa kike wasiendelee kukeketwa ,lakini bado jamii zetu hazituelewi tunaendelea kuwaelimisha ili nao wabadilike."- Mzee wa Kimila (Aliyesimama). Bado kuna kazi kubwa ya kumaliza swala la ukeketaji lakini kupitia elimu mbalimbali na mafunzo yanayotelewa kuhusu maswala ya ukeketaji juu ya hasara na madhara yake inaendelea kupunguza idadi ya wanaokeketwa.
"Kwa Tarime mwanamke kupigwa na kuvuliwa nguo hadhalani ilikuwa ni kitendo cha kawaida tu" - Sara Boniface (aliyesimama) , alielezea kwa kina kuhusu ukatili wa kupigwa ambapo aliongeza kwamba kwa sasa ukatili huo umepungua kutokana na elimu wanayoipata wanajamii juu ya ukatili wa kijinsia.
Mmoja wa wazee wa Kimira kutoka Tarime(aliyesimama) akieleza juu ya ukeketaji na kudai kuwa mwanamke aliyekeketwa anakuwa na thamani kubwa kama ilivyo kwa mwanamke mweupe kwa wasukuma, hii ni moja ya sababu zinazosababisha ukeketaji uendelee. Ikiwa elimu itaendelea kutolewa ukeketaji huu utapungua kwa kiasi kikubwa.
 "Ukatili wa ukeketaji ulikuwa unafanyika hadharani  kweupe, wazazi walikuwa wanalazimisha mabinti zao kukeketwa ili wapate mahali nyingi zaidi, ambapo fedha hizo ziwasaidie katika kupata kipato zaidi" - Nyakerandi Mariba. Swala hili limepungua sana kutokana na juhudi za wanamabadiliko kuendelea kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia.
"Maswala ya ukatili wa kijinsia yanaleta madhara makubwa katika jamii zetu,hasa kwa mabinti na akina  mama"-Lucy Matemba Afisa maendeleo ya jamii Tarime
Meneja wa kampeni ya Tunaweza Bi. Eunice Mayengela akiendelea kutoa Muongozo wa majadiliano
Wanamabadiliko wakiendelea kufuatilia mjadala
"Kila wiki tunapokea kesi zaidi ya kumi (10) zanazoripotiwa Tarime zikihusu kipigo,ubakaji, ulawiti na wanawake kutishiwa kuuwa,kupigwa sana kisha kubakwa kwa lazima ama kulawitiwa"- Dawati la Jinsia . Licha ya kesi hizo kuwa nyingi lakini elimu inayoendelea kutolewa na kampeni ya tunaweza imesaidia sana kupunguza ukatili wa kijinsia.
Wazee wa Kimila kutoka Tarime wakiteta jambo wakati wa mjadala
 Wanamabadiliko wakiwa katika picha ya pamoja.
Picha na Fredy Njeje

ALIYEMNAJISI MTOTO WAKE HADI KIFO, APEWA SHTAKA LA MAUAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mtoto Mase Denis kutoka Kabwana wilayani Rorya mkoani Mara aliyedaiwa kunajisiwa na baba yake wa kufikia Machi 3, mwaka huu alifariki dunia wakati akiwa njiani kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Rufani Bugando jijini Mwanza juzi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime-Rorya, Henry Mwaibambe aliwaambia waandishi wa habari kuwa awali mtuhumiwa Denis Ondigo alishitakiwa kwa kunajisi lakini kutokana na kifo hicho amebadilishiwa kuwa shtaka la mauaji.

Mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo majira ya saa 6 mchana wa Machi 3 akiwa nyumbani kwake Kabwana  baada ya mama wa mtoto kuwa amekwenda dukani kununua mahitaji ya nyumbani.

Kamanda huyo alisema Ondigo (26) mkazi wa Kabwana alifikishwa Mahakama ya Wilaya Tarime mkoani Mara kwa mara ya kwanza Machi 13.

FASTJET YAWEZESHA MADAKTARI KUSAFIRI KUTOA HUDUMA YA AFYA YA KINYWA NA MENO BURE KWA WANANCHI WILAYANI TARIME

 AQ6A7818.jpg
 Baadhi ya Madaktari watoa huduma ya meno na kimywa  pamoja na  watumishi wa Fastjet wakiwa wamewasili jijini Mwanza wakitokea Dar es salaam.
 AQ6A7930.jpg
 AQ6A7945.jpg
 Madaktari kutoka chama cha madaktari wa kinywa na meno Tanzania wakiwa wilayani tarime mkoa wa mara kuendelea kutoa elimu ya kinywa na meno ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno Duniani, ambapo walikuwa wanatoa huduma za uchunguzi,matibabu na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafikia wanafunzi na watoto yatima.AQ6A7949.jpg
Msemaji wa Fastjet Tanzania Bi. Lucy Mbogoro akiwapatia wanafunzi dawa za mswaki pamoja na miswaki kwa ajili ya kuendelea kuweka meno yao safi pamoja na vinywa vyao.
 AQ6A7959.jpg
Mmoja wa madakrtari wa meno na kinywa akiendelea kutoa elimu kwa wanafunzi.
AQ6A8009.jpg
Mh. Mariam  Mkono, Diwani wa Viti Maalum akizungumza na madaktari wa kinywa na meno kijijini Nyamwaga. 
 AQ6A8014.jpg
Debora Magasi, Muuguzi Mkuu wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya akizungumza na madaktari wa kinywa na meno kijijini Nyamwaga
AQ6A8020.jpg
Mganga Mkuu wa Kinywa na Meno wa Mkoawa Mara, Dkt Nila Jackson, alisema kati ya Machi 13 hadi 16 mwaka huu madaktari hao walifikia jumla ya wananchi 710  katika kijiji cha Nyamwaga wakiwemo wanafunzi 510 kutoka shule za msingi saba kijijini humo.
AQ6A8024.jpg

Raiswa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania Dkt. Ambege Jack Mwakatobe, alitoa wito kwa madaktari wa mikoa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi angalau mara mbili kwa mwezi ili kuwaongezea ufahamu na uelewa wananchi juu yausafi wa kinywa.

***********
SHIRIKA la Ndege la Fastjet limewezesha Madaktari wa kinywa na meno kusafiri kwenda kutoa huduma ya afya ya kinywa na meno bure kwa wananchi wa wilaya ni Tarime mkoani Mara.



Madaktari kutokachama cha madaktari wa kinywa na meno Tanzania wameanza ziara ya kujitolea katika wilaya ya Tarime mkoani mara ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno duniani ambapo watatoa huduma zauchunguzi, matibabu na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafikia wanafunzi na watoto yatima.



Akizungumza hivi karibuni wilayani Tarime, Daktari wa Meno wa Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Dk. David Mapunda, alisema ziara hiyo itawapatia fursa madaktari hao kufanya uchunguzi wa kinywa pamoja na kutoa huduma za matibabu pamoja na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Alisema miongoni mwa magonjwa yanayosumbua katika kinywa ni pamoja nakuoza kwa meno na ugonjwa wa fizi ambayo yanasababishwa na uchafu unaotokana na kutokupiga mswaki, kukosea kupiga mswaki au kutumia mswakiusio faa.

Alisema ili wananchi waepukane na magonjwa hayo ya meno wanapaswa kupiga mswaki angalau mara mbili kwa siku na kujenga utaratibu wa kuangalia afya ya kinywa na meno mara kwa mara.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Kinywa na Meno wa Mkoawa Mara, Dkt Nila Jackson, alisema kati ya Machi13 hadi 16 mwaka huu madaktari hao walifikia jumla ya wananchi 710 katika kijiji cha Nyamwaga wakiwemo wanafunzi 510 kutoka shule zamsingi saba kijijini humo.

"Kati ya tarehe hizo Madaktari hao  walitoa uchunguzi, matibabu na elimu ya afya ya kinywa na meno na kati ya tarehe 17 hadi 20 watakuwa katika wilaya ya Tarime na Rorya kuendelea na zoezi hilo," aliongeza Dk.Jackson

Naye Raiswa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania (Tanzania Dental Association), Dkt. Ambege Jack Mwakatobe, alitaja kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya kinywa na meno Duniani inayosema “Sema ah, fikiri akinywa, fikiria afya” ambayo inalenga kuwahamasisha wananchi kuzingatia afya ya kinywa na meno ilikujikinga na magonjwa yanayohusiana na ugonjwa wa meno ikiwemo magonjwa yakisukari na mengine.

Aidha alitoa wito kwa madaktari wa mikoa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi angalau mara mbili kwa mwezi ili kuwaongezea ufahamu na uelewa wananchi juu ya usafi wa kinywa.

Akizungumza kutoka kijiji cha Nyamwaga, Msemaji wafastjet nchini, Lucy Mbogoro,  alisema shirika la fastjet linafuraha kuwa sehemu ya shughuli hii inayofanywa na madaktari hawa wazalendo.

"Shirika la fastjet limewawezesha madaktari hawa kusafirikutoka Dar es salaam hadi Mwanza na kurudi ikiwa ni sehemu yampango wake wakurudisha shukrani kwajamii," alisema.

 
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa