VIONGOZI WA TAASISI, NA WAHALMASHAURI ZOTE MBILI WATETA NA MKUU WA WILAYA.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge siku ya tarehe 25/3/2025 amefanya kikao kazi na viongozi wa Halmashauri zote mbili pamoja na wa taasisi za serikali zilizopo katika Wilaya ya Bunda.Mh.Kaminyoge alisema lengo kuu la kikao hiki ni kujitambulisha kwenu nikiwa ndiye Mkuu wa Wilaya hii baada ya mabadiliko yaliyofanywa na Mh. Rais siku chache zilizopita, na pia kuwatambua nyie viongozi wote mliopo mahali hapa, pamoja na kuomba ushirikiano wenu ili tuweze kufanya kazi kwa pamoja na ushirikiano katika kuhakikisha tunawaletea wananchi wa Wilaya hii maendeleo na kuhakikisha wanaishi kwa amani, furaha na usalama.Katika kikao hicho viongozi...

KUTOKA BUNDA: WENYEVITI WA VIJIJI NA MTAA MARUFUKU KUMILIKI MUHURI.

Katika kikao cha mkutano wa Halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bunda kilichofanyika siku ya tarehe 20/3/2025 katika ukumbi wa Malaika, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge alisoma waraka wenye muongozo unaokataza wenyeviti wa vijiji na mitaa kumiliki muhuri.Lengo la kusoma waraka huo ni baada ya wenyeviti wa vijiji na mitaa kuomba kumiliki muhuri hiyo kama kitendea kazi chao, kitu ambacho Mkuu wa Wilaya ilibidi kusoma waraka huo ambao umeelezea na kutolea ufafanuzi kwanini hawapaswi kuwa nao na vifaa ambavyo wanatakiwa kuwa navyo kama sehemu ya vitendea kazi.Mh.Kaminyoge alisema wajibu wa mwenyekiti wa MTAA...

ASANTENI NA KWAHERINI HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru, 2024 ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava siku ya tarehe 3/8/2024 aliwashukuru Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa mapokezi mazuri waliyoyapata.Ndugu Mnzava alikiri kupokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney kuhusiana na mkesha wa Mbio za Mwenge, na shughuli zote zilizofanyika wakati wa mkesha.Pia, alishauri wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuhakikisha wanapima afya zao mara kwa mara na kuwa na mazoea ya kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao.TUNZA MAZINGIRA NA SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA TAIFA ENDELE...

MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney siku ya tarehe 2/8/2024 akipokea Mwenge wa uhuru katika viwanja vya shule ya msingi Nyamuswa B, kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Mh. Moses Kaigele.Mh Dkt Anney amesema Mwenge wa uhuru utakimbizwa km 109 na utatembelea, kukagua na kuzindua miradi nane ya maendeleo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, yenye thamani ya Tshs bilioni 2,312,165,470.&nb...

MWENGE WA UHURU, 2024 WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALAMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Mwenge wa uhuru, 2024 umezindua miradi minne ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, siku ya tarehe 2/8/2024.Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava amezindua mradi wa huduma za jamii, ambayo ni nyumba ya kulala wageni yenye thamani ya Tshs million 230 iliyopo Nyamuswa.Pia, alizindua nyumba ya watumishi (3in1), iliyopo Kata ya Hunyari katika kituo cha Afya Hunyari na shule ya Sekondari ya Mariwanda, na mradi wa maji Sanzante.Ndugu Mnzava alisisitiza wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuhakikisha wanashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha wanaenda kupiga kura ili waweze kuchangua viongozi...

MOTISHA YATOLEWA KWA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI, KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Dkt Vicent Anney ametoa ngao za motisha kwa Wakuu wa shule za Sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mh. Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi Mhe. Mtambi alizitaka shule ambazo zimefanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha Nne mwaka 2023 kuhakikisha wanapewa ngao yenye kuwaongezea motisha zaidi ili waweze kuongeza juhudi katika ufundishaji wa watoto shuleni, na kwa zile shule ambazo hazikufanya vizuri pia, wakuu wa shule wapewe vinyago ambavyo wataviweka katika ofisi zao ili kuongeza motisha ya ufundishaji katika shule.Kupitia hafla hiyo iliyofanyika tarehe...

RC MTAMBI, WANAHABARI NA WADAU WA MAENDELEO WALIVYOBEBA MDAHALO WA MARA BORA KWA UWEKEZAJI NA KUISHI

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi (katikati) akizungumza katika Mdahalo wa Mara Bora kwa Uwekezaji na Kuishi, mjini Musoma.  Wanaomsikiliza kwa makini ni Mwenyekiti wa MRPC, Mugini Jacob (wa pili kushoto), Katibu wa MRPC, Pendo Mwakyembe (kushoto), Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Mjanakheri Ibrahim (kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo sehemu ya Viwanda na Biashara, Gambaless Timotheo (wa pili kulia).------------------------------------------------------Na Christopher Gamaina, Musoma----------------------------------------------Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, waandishi wa habari na...

WANAMABADILIKO WASAIDIA KUPUNGUZA UKATILI WA KIJINSIA WILAYANI TARIME

"Shemeji zangu walikuwa sita walinipiga sana kwa kweli kwa sababu ya kutaka kumiliki Mali za Mume wangu ambaye ni Marehemu" , ni mmoja ya wanawake wa Tarime akisimlia  kwa masikitiko kutokana na ukatili alioupata baada ya kufiwa na mumewe, ambapo ndugu wa mume alilazimisha kumrithi yeye na mali za mumewe. Mila kama hizi zinazomkandamiza mwanamke zinapaswa kusitishwa  "Tumekubali kabisa watoto wetu wa kike wasiendelee kukeketwa ,lakini bado jamii zetu hazituelewi tunaendelea kuwaelimisha ili nao wabadilike."- Mzee wa Kimila (Aliyesimama). Bado kuna kazi kubwa ya kumaliza swala la ukeketaji lakini kupitia elimu mbalimbali na mafunzo...

ALIYEMNAJISI MTOTO WAKE HADI KIFO, APEWA SHTAKA LA MAUAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Mtoto Mase Denis kutoka Kabwana wilayani Rorya mkoani Mara aliyedaiwa kunajisiwa na baba yake wa kufikia Machi 3, mwaka huu alifariki dunia wakati akiwa njiani kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Rufani Bugando jijini Mwanza juzi. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime-Rorya, Henry Mwaibambe aliwaambia waandishi wa habari kuwa awali mtuhumiwa Denis Ondigo alishitakiwa kwa kunajisi lakini kutokana na kifo hicho amebadilishiwa kuwa shtaka la mauaji. Mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo...

FASTJET YAWEZESHA MADAKTARI KUSAFIRI KUTOA HUDUMA YA AFYA YA KINYWA NA MENO BURE KWA WANANCHI WILAYANI TARIME

   Baadhi ya Madaktari watoa huduma ya meno na kimywa  pamoja na  watumishi wa Fastjet wakiwa wamewasili jijini Mwanza wakitokea Dar es salaam.      Madaktari kutoka chama cha madaktari wa kinywa na meno Tanzania wakiwa wilayani tarime mkoa wa mara kuendelea kutoa elimu ya kinywa na meno ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya afya ya kinywa na meno Duniani, ambapo walikuwa wanatoa huduma za uchunguzi,matibabu na elimu kwa wakazi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafikia wanafunzi na watoto yatima. Msemaji wa Fastjet Tanzania Bi. Lucy Mbogoro akiwapatia wanafunzi dawa za mswaki pamoja na miswaki...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa