Home » » Mmoja auawa kwa kukatwakatwa kwa panga harusini wilayani Tarime

Mmoja auawa kwa kukatwakatwa kwa panga harusini wilayani Tarime

Mkazi mmoja wa Kijiji cha Kwisarara  katika Kata ya Bumera, wilyani Tarime, ameuawa kwa kukatwa mapanga wakati wakiwa kwenye sherehe ya arusi nyumbani kwa  mkazi mwingine wa kijiji hicho.

Ofisa Mtendaji wa Kata ya Bumera, Sospiter Marumi alimtaja aliyeuawa kuwa ni Mwita Kawawa (25).

Alisema mauaji hayo yamefanywa na mkazi mmoja wa Kijiji cha Kitenga.

Alisema chanzo cha mauaji  ni kupishana lugha kati ya watu hao wawili wakati wakicheza disko.

 Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Maalumu wa Kipolisi Tarime/Rorya, Sweetbert Njewike, alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo ya Oktoba 26 mwaka huu.

Njewike alisema ugomvi kati ya watu hao, ulikuja baada ya mtuhumiwa kumzuia Kawawa kuingia kwenye disko.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, mtuhumiwa huyo ameshakamatwa na kwamba atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka dhidi yake.

Aliwataka wananchi mkoani Mara, kuepuka kujichukulia sheria mikonono na kuathiri maisha ya watu wengine.

Kamanda Njewike alisema mara mara kwa mara wananchi mkoani humo wamekuwa wakijichukulia sheria mikononi kwa kuwaua wengine wasiokuwa na hatia.

Alisema polisi hawatasita kuchukua hatua dhidi ya watu wa aina hiyo, ili kukomesha vitendo visivyokubalika katika jamiii.

CHANZO MWANANCHI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa