Home » » TIB YAKOPESHA MATREKTA MATATU

TIB YAKOPESHA MATREKTA MATATU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

BENKI ya Uwekezaji Tanzania (TIB) imekopesha matrekta matatu yenye thamani ya sh milioni 83 kwa wanachama watatu wa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Chiringe kilichoko mjini Bunda, Mara ili walime kisasa na kuinua uchumi.
Waliopata matrekta hayo ni Robert Masatu, Opigi Ocharo na Nyerere Odera wote wakazi wa Bunda ambao watarejesha mkopo huo kwa miaka minne.
Mkopo huo ulikabidhiwa mjini hapa jana na Ofisa Ushirika wa wilaya hiyo, Saulo Lunyeka na kusema umetolewa na benki hiyo ili walime kwa ufanisi badala ya kilimo cha jembe la mkono.
Aliwaasa wanachama hao kurejesha mkopo huo kwa muda muafaka ili wengine wakope, huku akiwataka wananchi kujiunga kwenye vikundi wapate fursa ya kukopeshwa.
Mwenyekiti wa chama hicho, Robert Masatu, alisema walianza kuomba mkopo huo mwaka 2012 na kwamba matrekta hayo yatawasaidia wakulima wenye mashamba makubwa.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa