MADIWANI wanaojiita
kundi la okoa Rorya lenye muungano wa baadhi ya Madiwani wa Chama cha CCM
na Vyama vya wapinzani wamesema kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya Elias Goroi ni
Kiongozi mchapa kazi hivyo wanaotaka ahamishwe wana njama ya kurudisha nyuma
maendeleo Rorya.
Madiwani hao
waliokutana jana viwanja vya halmashauri ya Wilaya ya Rorya wamesema kuwa
wanasikitika kwa kauli ya Mwenyekiti wa Chama cha CCM Wilaya ya Rorya Samwel
Keboye (namba tatu) kwenye vyombovya habari kudai kuwa wananchi na Madiwani
wameandamana kutaka Dc Goroi ahamishwe.
Madiwani
wamekanusha kuwa hakuna maandamano ya wananchi wala Madiwani
yaliyofanyika nakwamba Dc Goroi na Mkurugenzi wa halmashauri Ephraem Ole
Nguyaine hawapaswi kuhamishwa kwakuwa wamesaidia kuwawajibisha watumishi wabovu
wanaojihusisha na ubadhilifu wa mali za umma na kuimalisha utawala bora.
Pendo odelle Diwani
wa Viti maalum Tarafa ya Nyancha (ccm)ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa
na mjumbe halmashauri ya ccm Wilayani hapo amemtaka mweyekiti wa CCM
Keboye kutenda haki kwa usawa na siyo kuwa kibaraka na
kuegemea kutetea upande mmoja wa Mbunge kwa masalahi yake binafsi.
0 comments:
Post a Comment