WANANCHI katika Tarafa ya Kenkombyo wilaya ya Bunda,
mkoani Mara, wamesema kuwa kama wafugaji wanaolisha mazao yao hawatadhibitiwa
iko siku utatokea mgogoro mkubwa, pamona na ugomvi kati ya wafugaji na
wakulima.
Wananchi hao wameyasema hayo juzi katika kijiji
cha Kasahunga, kwenye kikao cha maendeleo kilichokuwa kimeandaliwa na mkuu wa
wilaya ya Bunda, Bw. Joshua Mirumbe na kusimamiwa na Kaimu Afisa Tarafa ya
Kenkombyo, Bw. Abiud Peter Jandwa.
Wamesema kuwa wafugaji wenye makundi makubwa ya
ng’ombe kutoka katika maeneo mbalimbali, wamekuwa wakivamia mashamba yao na
kulisha mazao, na kwamba kama hali hiyo itadhibitiwa mapema inaweza kusababisha
mapigano kwa pande hizo mbili.
Wameongeza kuwa wafugaji hao kutokana na kukosa sehemu
ya kulisha mifugo yao kwa sababu ya ukame wamekuwa wakitoka maeneo
mbalimbali na kuingiza kwa makusudi mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima
nyakati za usiku ama asubuhi, pindi wanapoona wenye mashamba hawako
karibu.
Hata hivyo wananchi hao wamesema kuwa migogoro hiyo
pia imekuwa ikisababishwa na baadhi ya viongozi wa ngazi ya kijiji na kata,
baada yua kuruhusu makundi makubwa ya mifugo kuingia kwenye vijiji vyao,
wakitokea vijiji vingine, baada ya kupewa chochote na wafugaji hao kwa maslahi
yao binafsi.
Wakichangia hoja hiyo wananchi hao wamesema kuwa ni
vema sheria na taratibu zikafutwa, ikiwa ni pamoja na kila kijiji kutenga
eneo lake la kuchungia mifugo, baadala ya maeneo mengi kutumika kwa kilimo,
kama ilivyo kwa sasa.
Wameongeza kuwa hali hiyo imekuwa ikisababisha
wafugaji wa vijiji vingine kuvamia mashamba ya wakulima na kufanya uhalibifu
mkunbwa wa mazao, ambapo hali hiyo ikiachwa iendelee, licha ya kutokea mapigano
kati ya wafugaji na wakulima, pia itasababisha upungufu mkubwa wa chakula.
Akizungumzia kero hiyo, kaimu Afisa Tarafa ya
Kenkombyo, Bw. Abiud Peter Jandwa, amesema kuwa amekuwa akipokea malalamiko
hayo kutoka kwa wakulima, ambapo amewaonya viongozi wanaoruhusu makundi makubwa
ya mifugo kuingia kwenye vijiji vyao na kusababishha kuwepo kwa migogoro hiyo.
Bw. Jandwa amewataka wafugaji wenye mifugo mingi
kupunguza mifugo yao kwa kuiuza na kununua chakula, ili waweze kubaki na mifugo
michache, ikilinganishwa na maeneo ya malisho yaliyopo kwwenye vijiji vyao.
Kikao hicho kilishirikisha viongozi kuanzia ngazi ya
kitongoji hadi tarafa, vyama vya siasa na wadau mbalimbali wa maendeleo katika
tarafa hiyo.
0 comments:
Post a Comment