Home » » Wachimbaji dhahabu wafunikwa kifusi na kufa papo hapo

Wachimbaji dhahabu wafunikwa kifusi na kufa papo hapo

WACHIMBAJI wadogowadogo wa dhahabu wawili wamekufa baada ya kufukiwa na kifusi wilayani Bunda, mkoani Mara.

Mwenyewkiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Bunda, Bw. Joshua Mirumbe jana amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kusema kuwa tukio hilo lilitokea juzi katika kijiji cha Kamkenga tarafa ya Serengeti wilayani hapa.

Ofisa tarafa ya Serengeti Bw. Jastine Rukaka, amewataja watu hao kuwa ni pamoja Pascal William, mkazi wa Kamkenga wilayani Bunda na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Robert, mkazi wa Mugumu wilayani Serengeti.

Bw. Rukaka amesema kuwa wakati watu hao wakiendelea kuchimba dhahabu, ghafula kifusi kiliporomoka na kuwafunika na kwamba mwenzao wa tatu yeye alinusurika kifo baada ya kufanikiwa kutoka nje ya shimo hilo.

Amesema kuwa tayari miili ya wachimbaji hao iliondolewa ndani ya shimo hilo a kutambuliwa na kwamba polisi walifika katika eneo la tukio na kushuhudia vifo vya watu hao

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa