KUTOKANA
na baadhi ya madiwani kujihusisha na biashara katika halmashauri zao, mkuu wa
mkoa wa Mara Bw. John Tupa, amewaonya madiwani wote mkoani humo, kuacha mara
moja tabia hiyo kwani ni kunyume na utaratibu wa uongozi.
Mkuu
huyo wa mkoa wa Mara ameyasema hayo jana kwenye kikao maalum cha baraza la
madiwani cha kujadili hoja za mkaguzi na mdhibiti mkuu wa fedha za serikali,
kilichofanyika mjini Bunda.
Katika
hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa wilaya ya Butiama, Bi.
Angelina Mabula, mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa baadhi ya madiwani wamekuwa
wakifanya biashara na halmashauri zao kwa kuchukua tenda za miradi mbalimbali
ya maendeleo.
Mkuu
wa mkoa amesema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababisha miradi husika kutokuwa na
kiwango kinachotakiwa ikilinganishwa na fedha zilizotengwa, sanjari na miradi
kutokamilika kwa wakati uliopangwa.
Hata
hivyo mkuu wa mkoa wa Mara ameipongeza halmashauri hiyo kupata hati
inayoridhisha, lakini hakaonya kuwa sio vizuri kuwa na hoja za ukaguzi
zinazojirudia mara kwa mara katika halmashauri hiyo.
Katika
kikao hicho madiwani wameshangazwa na ujenzi wa ofisi za kata kutokukamilika
kwa wakati, ikiwa ni pamoja na soko la mji mdogo wa Kibara kutokukamilika,
ambapo fedha sh. milioni 10 zinadaiwa zimetafunwa katika mazingira ya
kutatanisha.
Hata
hivyo mratibu wa mradi wa TASAF wilayani Bunda, Bw. Mshingi Baragi amekanusha
tuhuma hizo na kusema kuwa fedha zote za mradi wa soko hilo zilipelekwa na
kufanya kazi iliyokusudiwa na kwamba kazi ya mradi huo imekamilika kama
ilivyokuwa imepangwa na kuongeza kuwa kinachotakiwa sasa ni wananchi kujenga
vibanda kwa ajili ya kuzunguka soko hilo.
Akihahirisha
kikao hicho mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bunda, Bw. Joseph Marimbe,
amesema kuwa watahakikisha kasoro zote zinaondolewa kadiri ya uwezo wao kwa
sababu hakuna sababu ya hoja za ukaguzi kujirudiarudia mara kwa mara.
Bw.
Marime amesema kuwa pale ambapo itawezekana kufanya vibaya watachukuliana hatua
kwa wale wanaohusika, kwa sababu hakuna haja ya hoja hizo kujirudiarudia mara
kwa mara.
0 comments:
Post a Comment