Home »
» Familia kuwaburuza kortini askari TANAPA
Familia kuwaburuza kortini askari TANAPA
|
|
FAMILIA ya marehemu Peter Maseya imekusudia kuwaburuza
mahakamani askari wa Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) katika Hifadhi ya
Serengeti kwa madai ya kumuua ndugu yao kwa tuhuma za ujangili.
Mauaji hayo yanadaiwa kufanywa usiku wa kuamkia Oktoba 16, mwaka huu
na askari hao baada ya kumvamia nyumbani kwake, kumteka na kumtesa
hadi kumuua akiwa kijijini kwake Murito-Nyamongo, wilayani Tarime,
Mara.
Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Chacha Masero,
alisema wanachosubiri sasa ni kukamilisha ushauri wa kisheria pamoja na
kupata majibu ya uchunguzi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala
Bora.
“Familia inaendelea kukamilisha hatua za kisheria za kuwafikisha
mahakamani askari waliofanya mauaji ya ndugu yetu… lakini pia
tunasubiri majibu ya kichunguzi yanayofanywa na Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora kupitia viongozi wake wakubwa ambao
tuliwaeleza tukio zima,” alisema Masero.
Akisimulia mkasa huo, Masero alisema Maseya alivamiwa akiwa nyumbani
kwake saa nane usiku, Oktoba 13, mwaka huu na askari hao wapatao watano
ambao walimchukua pamoja na watoto wake watatu na mfanyakazi wake.
“Askari hao walimtesa baba yetu, mmoja wao alitufuata na kutueleza
kuwa baba hataki kusema na kutuambia twende tukapewe urithi wetu
kabisa,” alisema.
CHANZO;TANZANIA DAIMA
|
|
0 comments:
Post a Comment