Home » » ‘Tutaendeleza mradi’

‘Tutaendeleza mradi’

.Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, wameahidi kushirikiana na wakazi wa wilaya hiyo, katika kuufanya endelevu, mradi wa chakula cha wanafunzi shuleni hata baada ya wafadhili kuondoka.
Mradi huo unaoendeshwa katika Wilaya za Bunda na Butiama za mkoani Mara, umekuwa ukifadhiliwa na Shirika la PCI la Marekanitangu mwaka 2010 ambalo linatarajia kumaliza shughuli zake mwaka 2016.
Wakizungumza katika warsha maalum iliyoandaliwa na shirika hilo, madiwani walisema maadam mradi huo umeonyesha mapinduzi makubwa katika elimu kuna kila sababu ya halmashauri kuuendeleza.
Waliyataja baadhi ya mapinduzi hayo kuwa ni ongezeko la ufaulu wa wanafunzi, mahudhurio na uandikishaji wa wanaoanza masomo ya darasa la kwanza.
Madiwani hao walisema watatenga fungu kwenye bajeti ya halmashauri hiyo kwa lengo la kuboresha miundombinu ya shule huku wakiitaka jamii kuchangia vyakula.
Walisema hatua hiyo ni ya muhimu katika kuboresha sekta ya elimu katika halmashauri hiyo.
CHANZO;MWANANCHI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa