Home » » MWENYEKITI WA KIJIJI RORYA MBARONI WIZI WA NG'OMBE

MWENYEKITI WA KIJIJI RORYA MBARONI WIZI WA NG'OMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
JESHI la Polisi Rorya linamshikilia Mwenyekiti wa Kijiji cha Marasibora, Kata ya Kisumwa, Sproza Charles, kwa tuhuma za wizi wa ng’ombe watatu wa ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Arusha, Aden Kagose.
Mwenyekiti huyo alifikishwa katika kituo cha Polisi Komoswa jana baada ya kudaiwa kushirikiana na wenzake watatu ambao ni Hamis Nyamaganda, Mwita Mwita na Werema Nyamaganda wakazi wa Marasibora, kuiba ng’ombe hao.
Watuhumiwa Nyamaganda na Werema wanaendelea kusakwa na polisi baada ya kutorokea kusikojulikana.
Kamanda wa Polisi Mkoa,  Justus Kamugisha, aliwaambia waandshi wa habari kwamba mwenyekiti wa kijiji hicho aliingia kwenye tuhuma hiyo baada ya kuidhinisha barua ya kuhalalisha ng’ombe hao wa wizi kuuziwa Mwita.
Alisema mwenyekiti huyo aliidhinisha barua ya kuuzwa ng’ombe hao wenye thamani ya sh 1,800,000 kutoka kwa watuhumiwa Matiko Nyamaganda na Werema Nyamaganda bila kuthibitisha uhalali wa umiliki wake.
Jeshi hilo lilifanikiwa kuwakamata mwenyekiti na Mwita muda mfupi na kufikishwa kituo cha Polisi cha Komaswa ambapo watafikishwa mahakamani kesho.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, mmiliki wa ng’ombe hao, Kagose, alikiri kuibwa ng’ombe hao na kwamba anasubiri taratibu za kisheria kufuatwa ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani.
Kagose anayewakilishwa na ndugu yake katika suala hilo, alisema alipewa taarifa  ng’ombe wake wameibiwa na watu hao.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa