Home » » WAZAZI TARIME WACHARUKA MCHANGO WA SH. 1000 SHULE ZA MSINGI

WAZAZI TARIME WACHARUKA MCHANGO WA SH. 1000 SHULE ZA MSINGI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mchango wa shilingi elfu moja Mzazi kwa ajili ya Ujenzi wa Choo  katika Shule ya Msingi Sirari Wilayani Tarime Mkoani Mara umekuwa  kizaa zaa ktika Mkutano wa Serikali ya Kijiji uliofanyika jana katika Shule hiyo.

Baadhi ya Wazazi hao wameshindwa kulipa kiwango hicho  kwa ajili ya kusukuma gurudumu la Maendeleo katika Shule hiyo,suala ambalo lilipelekea jana kuongeza adhabu ya kulipa shilingi elfu kumi kwa mtu ambaye alikuwa hajalipa shilingi elfu moja hapo awali.

Shule ya Msingi Sirari inakumbwa changamoto ya Upungufu wa  vyoo suala amabalo ni Changamoto kubwa  kwa Wanafunzi hao.

Kupitia Mkutano mkuu wa Serikali amabao ulifanyika uliadhimia kuchanga Shilingi elfu Moja kwa ajili ya ujenzi wa Choo cha Shule ya Msingi suala ambalo limepelekea jana  Wazazi  ambao hawajakamilisha Mchango wa kulipa faini ya Shilimngi Elfu kumi uku ikiundwa kamati ya Wajumbe Sita ya kupitia Michango katika vijiji na vitongoji kwa lengo la kubaini wananchi waliogomea Michango hiyo.

Hata hivyo wazazi hao katika Mkutano huo wamemtaka Mwl mkuu wa Shule ya Msingi Sirari kuwasomea Mapato na Matumizi kwani hapo awali Bodi ya Shule ilikuwa ikichangisha Michango bila kushirikisha Serikali ya Kijiji na ndipo waliweza kusimamishwa zoezi hilo la kuchangisha Michango hiyo baada ya Malalamiko kutoka kwa wazazi.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Kijiji  Nyangoko Paul kupitia Mkutano huo amewataka wenyeviti wote wa Vitongoji kutoa Ushirikiano wa kutosha kwa lengo la kubaini wale wote waliogoma kuchanga Mchango huo.

Sanjari na hayo Mwenyekiti huyo amewataka Wananchi hao kuondokana na kuchagua Viongozi kwa ushabiki na hatimayake wanashindwa kutoa Ushirikiano katika Utendaji wa kazi.

Suala la kushangaza na kuonesha kuwa jamii hjaitaki kujitolea mpaka kusukumwa baada ya kikao hicho gradio Victoria hili lilifanikiwa kutembelea ofisi ya Ofisa Mtendaji wa kata ya Sirari nakushudia Mamia ya watu wakiwea kwenye Mstali wa kulipa shilingi elfu moja kwa kuogopa faini ya Shilingi Elfu kumi iliyoazimiwa na Mkutano huo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa