Home » » 'SERIKALI ISITISHE POSHO BUNGE LA KATIBA'

'SERIKALI ISITISHE POSHO BUNGE LA KATIBA'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Makamu wa Rais wa Vyama vya Walipa Kodi Duniani, Otieno IgogoSERIKALI imeombwa kuzuia malipo ya posho kwa wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba, badala yake fedha hizo zielekezwe katika huduma za jamii.

Kauli hiyo ilitolewa juzi wilayani Rorya mkoani Mara na Makamu wa Rais wa Vyama vya Walipa Kodi Duniani, Otieno Igogo, alipokutana na wafanyakazi wa Shamba la Masista wa Baraki.
Igogo amesema hakuna sababu kwa serikali kutumia fedha za walipa kodi kuwalipa wabunge hao ambao imedhihirika wazi kuwa hawawezi kuwapatia Watanzania katiba bora waliyoitegemea.
“Tumeshuhudia kodi za Watanzania zikichezewa kwa kuendesha Bunge la Katiba lililojaa vijembe, matusi, kejeli na ushabiki wa vyama.
“Hapa hakuna katiba mpya, badala yake ni vema serikali ikazitumika kuokoa maisha ya wananchi kwa kununua dawa na vifaa tiba  katika vituo vya afya maeneo ya vijijini nchini,” alisema.
Shutuma za kiongozi huyo zimekuja kukiwa na shutuma kutoka kila kona ya nchi, juu ya mwenendo mzima wa Bunge hilo ulivyokwenda.
Akitoa taarifa za shamba hilo linaloendesha shughuli za kilimo na  ufugaji, mkuu wa shamba hilo, Sista Janepher Mabonyesho, amesema kuwa pamoja na  kituo hicho  kutoa mchango mkubwa wa maendeleo, lakini  hakuna msaada wowote unatolewa na serikali kuunga mkono juhudi hizo.
Awali Paroko wa Parokia ya Baraki, Padri  Alexander Choka, ameitaka jamii kuacha  kuilalamikia serikali kwa  kila kitu bali watambua wajibu wao wa kufanya kazi kwa bidii.
Akiwa katika shamba hilo, makamu huyo wa rais  wa vyama vya walipa kodi dunia, mbali na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na kituo hicho, imezindua tovuti na kutoa sh milioni 6 kwa ajili ya kusaidia kituo hicho na chakula cha mwezi mzima kwa kituo cha watoto wadogo katika kituo hicho.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa