Home » » WAFANYA BIASHARA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA BIASHARA

WAFANYA BIASHARA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA BIASHARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAFANYABIASHARA wadogo hapa nchini wametakiwa kuchangamkia fursa za biashara zinazotolewa na Kampuniya China World Buz iliyoanzishwa naWatanzania waishio nchini China, itakayowawezesha kuagiza bidhaa mbalimbali kwa mtaji kidogo walionao bila kuingia gharama ya kufuata bidhaa hizo nchini China.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Bw.Justine Luvanda wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akitambulisha mradi huo katika mikoa mitatu hapa nchini.
Alisema kuwa,lengola mpango huo ni kuwawezesha Watanzania wenye mtaji kidogo kukuza mitaji yao kwa kuagiza bidhaa kutoka China bila kuingia gharama ya kwenda kununua bidhaa hizo China kutokana na mitaji yao.
Bw.Luvanda alisema kuwa iwapo elimu itawafikia wafanyabiashara hao itaweza kuwanufaisha kwa kiasi kikubwa kwani baadhi yao wamekuwa na mitaji midogo na kushindwa kujua wafanyebiashara gani kwa ajili ya kukuza biashara zao.
Aliongeza kuwa,kupitia mpango huo wakibiashara wafanyabiashara hao wataweza kuletewa bidhaa zao kutoka China na kwa bei nafuu na kuuza nchini na kupata faida nzuri kwa kuongezea mitajiya o.
Alifafanua kuwa, kupitia kampuni hiyo wataweza kupata elimu jinsi ya kufanyabiashara zao na kuku zamitaji yao na kuwa na uhakika na usalama wa bidhaa zao kwani pindi itakapotokea hasara yoyote katika uagizaji wa biashara hizo zitalipwa na kampuni hiyo.
Naye afisa mtendaji mkuu wa kampuni hiyo hapa Tanzania Bw.Shafii Swed alisema kuwa, kampuni hiyo ni kampuni ya kwanza ya kitanzania kupata usajili wakibiashara
na ilifunguliwa rasmi na Rais wa China Xijin Ping kuwa eneo huru la soko la kimataifa la biashara.
Alisema kuwa, kampuni hiyo ilifunguliwa ikiwa na lengo la kukuza na kuendeleza mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na China ikiwa na lengo la kutoa bidhaa China na kuziuza Tanzania huku wakichukua mali ghali na kupeleka nchini China hali ambayo itasaidia kukuza soko la ajira hapa nchini.
Akizungumzia changamoto wanayoipata wafanyabiashara kuanzishwa kwa kampuni hiyo wamedai kuwa kutokana na kero wanazop ata ikiwani pamoja na gharama za kufuatilia viza, usafiri, malazi na gharama nyingine mbalimbali hivyo kupitia kampuni hiyo itawawezesha kuwarahisishia kupata bidhaa zao kwa wakati

Chanzo:Majira

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa