Home » » KIGOGO CCM TARIME MBARONI

KIGOGO CCM TARIME MBARONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Tarime na Rorya, linamshikilia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Rorya, Roger Kukuu kwa tuhuma za kujipatia sh milioni 11.5 kwa udanganyifu.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime na Rorya, Kamishina Msaidizi Mwandamizi, Justus Kamugisha, alisema kiongozi huyo anadaywa kujipatia fedha hizo kutoka kwa Paul Oyoo.
Alieleza kiongozi huyo alichukua fedha hizo kwa udanganyifu Januari 6 mwaka huu, baada ya kupata zabuni ya kutengeneza samani za Halmashauri ya Rorya, lakini alishindwa kurejesha fedha hizo kama alivyotakiwa.
 “Huyu mtu tunamshikilia kwa tuhuma za wizi wa kuaminika, kwani alipopata tenda (zabuni) za kutengeneza fenicha za halmashauri ya Rorya alichukua fedha kwa Paul Oyoi, lakini alipolipwa alishindwa kurejesha fedha hizo,”alisema Kamanda Kamugisha.
 Hata hivyo, alisema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Samwel Kiboye, alipozungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema chama hakihusiki kwa tukio hilo, hivyo kutaka vyombo vya dola kuchukua hatua bila kujali cheo cha mtu ili haki iweze kutendeka.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa