Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
“Ndugu wajumbe napenda kutumia nafasi hii kutangaza rasmi kwamba
ninagombea tena ubunge wa jimbo hili. Wale wanaokereka wakereke tu. Nina
nguvu bado za kuwatumikia Wanabunda.” Stephen Wassira
Mbunge wa Jimbo la Bunda (CCM), Stephen Wassira ametangaza kuwa
atatetea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao, huku akijigamba
kuwa yeye ni “mwarobaini wa matatizo” yanayowakabili wakazi wa jimbo
hilo.
Kabla ya kutangaza nia hiyo jana, mara kadhaa
Wassira amekuwa akihusishwa na suala la urais na ni mmoja wa makada sita
wa CCM ambao walipewa adhabu na chama hicho, Februari 18, mwaka huu
baada ya kukutwa na makosa ya kuanza mapema kampeni za urais mwaka 2015.
Wassira, ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais (Mahusiano na Uratibu) alitangaza uamuzi wake huo katika kikao cha
kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM wilayani Bunda kilichofanyika kwenye
ukumbi wa halmashauri ya wilaya hiyo.
Wassira, ambaye ana umri wa miaka 69, aliwaponda
wanaombeza kuwa amezeeka, hivyo kuweka wazi kwamba ameamua kuwania tena
nafasi hiyo kwa sababu bado ana nguvu na uwezo wa kuwatumikia wananchi
kwa kipindi kingine cha miaka mitano na kutimiza ndoto zao za kupata
maisha bora kwa kila mmoja wao.
“Ndugu wajumbe napenda kutumia nafasi hii
kutangaza rasmi kwamba ninagombea tena ubunge wa jimbo hili. Wale
wanaokereka wakereke tu. Nina nguvu bado za kuwatumikia
Wanabunda,”alisema Wassira.
“Nyote ni mashahidi kwa jinsi ninavyoshirikiana
nanyi katika kuondoa changamoto zinazotukabili ambazo nyingi ziko karibu
kuisha ili wote wapate maisha bora yaliyoahidiwa na CCM. Nawaombeni tu
tuzidi kushirikiana,” alisema Wassira, ambaye pia ni mjumbe wa
Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ya CCM.
Pamoja na mwanasiasa huyo mkongwe, ambaye amekuwa
waziri katika awamu tatu za urais, kujitahidi kwa kiasi kikubwa
kuwaletea wakazi wa jimbo hilo, bado kuna changamoto katika sekta za
afya, maji hasa kwa maeneo ya vijijini.
Wachunguzi wa mambo wanadai kuwa kama hatatimiza
ahadi hiyo aliyoitoa wakati wa kampeni za mwaka 2005 na kuanza ujenzi wa
mradi mkubwa wa maji wa mji huo mwaka 2007, basi huenda akapata wakati
mgumu kutetea nafasi hiyo.
Wassira anakuwa mwanachama wa kwanza wa CCM
kutangaza wazi nia yake ya kuwania nafasi hiyo. Wengine wanaotajwatajwa
kuuwinda ubunge huo ni mbunge wa viti maalumu (CCM), Ester Bulaya na
mjumbe wa NEC wa wilaya hiyo, Bonifasi Mwita ambao bado hawajaweka wazi
nia yao.
Wassira alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo chini ya
uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere na pia ameshawahi kuwa Naibu Waziri wa
Tawala za Mikoa na baadaye kuwa Waziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo
chini ya uongozi wa Ali Hassan Mwinyi.
Aliteuliwa kuwa Waziri wa Maji mwaka 2006 na
baadaye kuhamishiwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika na mwaka 2008
aliteuliwa kuwa Waziri wa Tamisemi. Mwaka 2010 Wassira aliteuliwa
kushika wadhifa alionao sasa.Mbunge wa Jimbo la Bunda (CCM), Stephen Wassira ametangaza kuwa
atatetea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao, huku akijigamba
kuwa yeye ni “mwarobaini wa matatizo” yanayowakabili wakazi wa jimbo
hilo.
Kabla ya kutangaza nia hiyo jana, mara kadhaa
Wassira amekuwa akihusishwa na suala la urais na ni mmoja wa makada sita
wa CCM ambao walipewa adhabu na chama hicho, Februari 18, mwaka huu
baada ya kukutwa na makosa ya kuanza mapema kampeni za urais mwaka 2015.
Wassira, ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais (Mahusiano na Uratibu) alitangaza uamuzi wake huo katika kikao cha
kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM wilayani Bunda kilichofanyika kwenye
ukumbi wa halmashauri ya wilaya hiyo.
Wassira, ambaye ana umri wa miaka 69, aliwaponda
wanaombeza kuwa amezeeka, hivyo kuweka wazi kwamba ameamua kuwania tena
nafasi hiyo kwa sababu bado ana nguvu na uwezo wa kuwatumikia wananchi
kwa kipindi kingine cha miaka mitano na kutimiza ndoto zao za kupata
maisha bora kwa kila mmoja wao.
“Ndugu wajumbe napenda kutumia nafasi hii
kutangaza rasmi kwamba ninagombea tena ubunge wa jimbo hili. Wale
wanaokereka wakereke tu. Nina nguvu bado za kuwatumikia
Wanabunda,”alisema Wassira.
“Nyote ni mashahidi kwa jinsi ninavyoshirikiana
nanyi katika kuondoa changamoto zinazotukabili ambazo nyingi ziko karibu
kuisha ili wote wapate maisha bora yaliyoahidiwa na CCM. Nawaombeni tu
tuzidi kushirikiana,” alisema Wassira, ambaye pia ni mjumbe wa
Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ya CCM.
Pamoja na mwanasiasa huyo mkongwe, ambaye amekuwa
waziri katika awamu tatu za urais, kujitahidi kwa kiasi kikubwa
kuwaletea wakazi wa jimbo hilo, bado kuna changamoto katika sekta za
afya, maji hasa kwa maeneo ya vijijini.
Wachunguzi wa mambo wanadai kuwa kama hatatimiza
ahadi hiyo aliyoitoa wakati wa kampeni za mwaka 2005 na kuanza ujenzi wa
mradi mkubwa wa maji wa mji huo mwaka 2007, basi huenda akapata wakati
mgumu kutetea nafasi hiyo.
Wassira anakuwa mwanachama wa kwanza wa CCM
kutangaza wazi nia yake ya kuwania nafasi hiyo. Wengine wanaotajwatajwa
kuuwinda ubunge huo ni mbunge wa viti maalumu (CCM), Ester Bulaya na
mjumbe wa NEC wa wilaya hiyo, Bonifasi Mwita ambao bado hawajaweka wazi
nia yao.
Wassira alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo chini ya
uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere na pia ameshawahi kuwa Naibu Waziri wa
Tawala za Mikoa na baadaye kuwa Waziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo
chini ya uongozi wa Ali Hassan Mwinyi.
Aliteuliwa kuwa Waziri wa Maji mwaka 2006 na
baadaye kuhamishiwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika na mwaka 2008
aliteuliwa kuwa Waziri wa Tamisemi. Mwaka 2010 Wassira aliteuliwa
kushika wadhifa alionao sasa.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment