Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamishna wa NCCR-Mageuzi Mkoa wa Mara, Stephen Sebeki ameuawa
kwa kukatwakatwa mapanga na mtu anayedaiwa kuwa ni hawara wa shemeji
yake, chanzo kikidaiwa kuwa ni mgogoro wa nyasi za kuezekea.
Mkuu wa polisi wa Wilaya ya Serengeti, Pius Mboko
alisema tukio hilo lilitokea jana saa 2:00 asubuhi katika Kijiji cha
Rung’abure wilayani hapa.
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho, Charles
Kibure alisema Sebeki aliuawa kwa kukatwa na panga sehemu ya shavu la
kushoto, kichwani kwa nyuma na kiganja cha mkono wa kushoto na kufariki
dunia papo hapo.
Mmoja wa ndugu wa marehemu alisema Sebeki aliuawa
baada ya shemeji yake (mke wa marehemu kaka yake) kuuza nyasi za Sebeki
alizokuwa amezipanda kwa kazi mbalimbali.
Inadaiwa kuwa Sebeki alipomhoji shemeji yake huyo sababu za kuuza nyasi zake, alitukanwa.
“Kumbe ndani kulikuwa na hawara yake amelala akatoka na panga na kuanza kumshambulia,” alisema Kibure.
Alisema baada ya tukio hilo mtuhumiwa na hawara yake walikimbia, huku wakiwaacha watoto watatu na haijajulikana walipo.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Jacob Sendi alisema mtuhumiwa kwa muda mrefu amekuwa akiishi na shemeji yake.
Alisema polisi walimchukua shemeji mkubwa wa
Sebeki, Mrembo Ngige ambaye alikuwapo wakati tukio hilo pamoja na watoto
hao watatu ili kusaidia upelelezi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment