Home » » UKATA WAITESA RIADHA MARA

UKATA WAITESA RIADHA MARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Timu ya riadha ya mkoa wa Mara huenda ikajitoa kushiriki kwenye mashindano ya taifa ya riadha yatakayofanyika Jumamosi na Jumapili jijini Dar es Salaam kutokana na kukosa Sh4 milioni za kufanikisha ushiriki wao.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mara, Dotto Bwire, kikosi hicho kilikuwa kiondoke jana mjini Musoma kwa basi kuja Dar es Salaam, lakini kimekwama kusafiri kutokana na kukosa nauli.
Bwire alisema wamehangaika kuomba misaada kwa wadau mbalimbali wa mkoa huo ikiwamo wabunge na wakurugenzi wa halmashauri zote nane za Mkoa wa Mara, lakini imeshindikana.
“Hadi sasa (jana jioni) hatuna hata senti tano, hatujui timu yetu itafikaje Dar es Salaam kwenye hayo mashindano, kama tutakwama basi hatuna budi kujitoa ingawa tutawanyong’onyeza wanariadha wetu ambao kwa kweli wamejiandaa,” alisema Bwire.
Mwenyekiti wa chama hicho, Daniel Thomas, ambaye pia ni miongoni mwa Watanganyika wa kwanza kushiriki Olimpiki, alisema kikosi hicho cha mkoa kilichochaguliwa kwenye mashindano ya mkoa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu Bunda kinaendelea na mazoezi.
Thomas alisema timu hiyo ni ya mbio ndefu za mita 10,000 na 5,000, mbio za kati mbio fupi, relay, miruko na mitupo.
Chanzo:Mwnanchi 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa