Home » » WAZIRI CHIKAWE AKIRI KOSA

WAZIRI CHIKAWE AKIRI KOSA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, amekiri mbele ya viongozi wa serikali za vijiji saba vinavyozunguka mgodi wa dhahabu wa North Mara, kuwa serikali ilifanya makosa na inastahili kulaumiwa kutokana na adha wanazopata wananchi toka mgodini.
Chikawe alifikia hatua hiyo jana baada ya kupokea taarifa ya malalamiko kutoka kwa viongozi wa serikali za vijiji na kata vya Nyamwaga, Genkuru, Kewanja, Nyakunguru, Kerende, Matongo na Nyangoto, ya kupigwa, kunyanyaswa, kuuawa, kujeruhiwa na kubambikwa kesi na polisi.
Pia waziri huyo alielezwa jinsi mgodi wa Kampuni ya Afrika Barrick ya Canada, ulivyoshindwa kuwafidia wananchi ili wahame na wale wote waliofanyiwa uthamini na kikosi kazi mwaka jana, katika vijiji vya Kewanja, Nyakunguru na Nyangoto, kuendelea kuwepo wakipata adha.
Malalamiko hayo kwa Chikawe aliyeambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu, yalitolewa Diwani wa Kata ya Kemambo, Willison Mangure na mwenzake wa viti maalum Matongo Tontora
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa