Home » » WAJERUHIWA WAKIGOMBANIA ARDHI

WAJERUHIWA WAKIGOMBANIA ARDHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WATU wawili wakazi wa Kijiji cha Sirorisimba katika Wilaya ya Butiama mkoani Mara, wamejeruhiwa kwa kuchomwa mishale, baada ya kutokea ugomvi wa kugombania ardhi kati yao na wakazi wa Kijiji cha Mikomariro cha wilayani Bunda.
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi wilayani Bunda, waliojeruhiwa ni Hamisi Nyamhanga (38) aliyechomwa na mshale mgongoni na Samson Wambura (36) aliyechomwa mshale mguuni, wote wakiwa ni wakazi wa kijiji cha Sirorisimba.
Mwenyekiti wa kijiji cha Sirorisimba, Alexander Makire, aliliambia gazeti ili jana kuwa tukio hilo limetokea juzi asubuhi baada ya wakazi wa kijiji cha Mikomariro kuvamia shamba la mkazi wa kijiji cha Sirorisimba na kuanza kulilima kwa kutumia jembe ya kukuotwa na ng’ombe.
Makire alisema kuwa baada ya mwenye shamba kuwaona watu hao wakilima, alikwenda kuwauliza kwanini wameamua kufanya hivyo, lakini badala yake watu hao waliamua kupiga yowe na watu wakakusanyika ndipo vurugu kubwa zilitokea.
“Majeruhi mmoja amejeruhiwa vibaya na amepelekwa katika hospitali ya mkoa mjini Musoma,” alisema afisa mmoja wa polisi ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake akidai si msemaji rasmi.
Kufuatia vurugu hizo, jeshi hilo kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya ya Bunda, walifika eneo la tukio na kuwatia mbaroni watu wawili, Tulubeth Tundula (32) na Juma Werema (45) ambao wote ni wakazi wa kijiji cha Mikomariro.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa