Home » » WANAFUNZI WAKATISHA MASOMO

WANAFUNZI WAKATISHA MASOMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
SHULE ya sekondari Hunyari iliyoko katika Wilaya ya Bunda mkoani Mara, inakabiliwa na changamoto ya utoro mkubwa wa wanafunzi kutokana na baadhi yao kukatisha masomo kwa kuo, kuolewa na wengine kuchunga mifugo.
Taarifa hiyo ilitolewa jana na mkuu wa shule hiyo, Joachim Kishai, mbele ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Wilaya ya Bunda, Boniphace Mwita aliyetembelea shule hiyo.
Kishai alisema kuwa shule hiyo yenye kidato cha kwanza hadi cha nne, inakabiliwa na changamoto hiyo ya utoro wa wanafunzi unaosababishwa  na baadhi yao kubeba mimba, kuoa, kuolewa na kufanya shughuli za uchungaji wa mifugo.
Alifafanua kuwa kwa mfano, wanafunzi wa kidato cha nne walianza kidato cha kwanza wakiwa 188, lakini hadi sasa wamebakia wanafunzi 44 tu.
Alisema kuwa kwa upande wa kidato cha tatu walioanza ni 280, lakini waliopo kwa sasa ni 104 na kidato cha pili walioanza ni 136 waliopo ni 121.
Aliongeza kuwa kuwa hali hiyo husababishwa na wazazi kutotilia umuhimu elimu kwa watoto wao, kwani baadhi yao uozwa ama kuoa, bila wazazi kuchukua hatua yoyote ile na kuona jambo hilo kama la kawaida tu.
Alisema kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule hiyo umekuwa ukichukuwa hatua, ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola ama mahakamani wazazi wa aina hiyo.
Naye Mwita, alisema kuwa watashirikiana na halmasahuri ya wilaya hiyo kupitia idara ya elimu kuanzisha opelesheni ya kuwasaka watoro.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa