Home » » WATAKA TEMBO WADUNGWE SINDANO

WATAKA TEMBO WADUNGWE SINDANO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
KUTOKANA na kero ya wanyama aina ya Tembo kushambulia mazao ya wananchi, na kuwaingizia hasara, wananchi wanaoishi pembezoni mwa Hifadhi ya Serengeti wilayani Bunda, wameiomba serikali kutafuta njia mbadala ya kudhibiti wanyama hao.
Wananchi hao wamependekeza wanayama hao kudungwa sindano za uzazi wa mpango ili wapunguze kuzaliana kutokana na wingi wao.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Boniphace Gitare, wananchi hao walisema kutokana na wingi wa tembo ni vyema serikali ichukue hatua madhubuti ya kuwazuia.
Walisema kuwa ni vyema wanyama hao hasa majike wakadungwe sindano za uzazi wa mpango ili wazae kwa majira na wapunguze kushambuli mazao ya wakulima na kutishia maisha yao.
“Tunaomba serikali itafute njia mbadala kudhibiti wanyama hawa kwa sababu ni wengi kupita kiasi na wanavamia kwenye makazi yetu, njia mojawapo tunapendekeza wadungwe sindano za uzazi wa mpango. Mbona binadamu wanachomwa sindano hizo,” alisema mwananchi mmoja wa kijiji cha Mariwanda.
Naye Gitare alisema wanyama hao ni rasilimali kwa taifa na kwamba ni kivutio kwa watalii wanaoingizia nchi mapato, hivyo aliwataka wananchi hao kuimarisha uhifadhi.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa