Home » » JESHI LA POLISI MKOA WA MARA NA NCHI JIRANI KENYA WAMEFANIKIWA KUWAKAMATA WATU WAWILI KWA TUHUMA ZA KUMWIBA MTOTO.

JESHI LA POLISI MKOA WA MARA NA NCHI JIRANI KENYA WAMEFANIKIWA KUWAKAMATA WATU WAWILI KWA TUHUMA ZA KUMWIBA MTOTO.

Jeshi la polisi mkoa wa Mara kwa kushirikiana na wenzao wa nchi jirani   ya Kenya wamefanikiwa kuwakamata watu wawili kwa tuhuma za   kumwiba mtoto Diana Meshack mwenye  umri wa miezi saba mkazi   wa makoko katika manispaa ya musoma kisha kuficha katika nchi hiyo  jirani huku waibaji hao wa mtoto wakiomba kupewa fedha kiasi cha  shilingi milioni tatu ili waweze kumrejesha motto huyo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara kamishna msaidizi wa jeshi la  polisi ACP Philip Alex Kalangi, amesema kuwa mfanyakazi wa ndani   Paulina Sobe alikula njama na kutoweka na mtoto huyo hadi nchini   Kenya kabla baadhi ya watuhimiwa hao kuanza kumpigia simu mama   mzazi wa mtoto Bi Gaudioza Meshack wakitaka kutoa kiasi cha shilingi  milioni tatu ili waweze kumrejesha mtoto huyo.
 
Kamanda Kalangi amewataja watuhumiwa ambao tayari   wamekamatwa wakiwa na mtoto huyo huku akisema mfanya kazi wa  ndani bado anatafutwa na kwamba taratibu zimefanyika za kuleta   watuhumiwa nchini kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
 
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la matukio ya  wizi wa watoto ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu   wakiwemo wafanyakazi wa ndani na baada kufanya vitendo hivyo   wameku wa wakilazimisha kupewa fedha kama moja sharti la kurejesha  watoto katika familia zao.
 Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa