Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Anna Nkinda – Tarime
Wanawake
wilayani Tarime wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya uchaguzi
mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwezi huu itakapofika na wachague viongozi watakaowaona
wanafaa ambao watawaletea maendeleo.
Rai hiyo imetolewa leo
na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati
akiongea na wanawake wa wilaya hiyo iliyopo mkoani Mara katika ukumbi wa
mikutano uliopo katika hoteli ya CMG.
Mama Kikwete ambaye ni Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Lindi mjini alisema
kupiga kura ni haki ya kila mtu hivyo basi haitakuwa busara kwa wanawake hao kuharibu kura zao kwa kukaa
majumbani siku ya uchaguzi ikifika bali waende kupiga kura katika vituo walivyojiandikisha
.
“Kura ni siri ya mtu,
wewe ndiye unayefahamu kiongozi gani wa kumchagua nawasihi chagueni viongozi
wazuri na siyo bora viongozi, wahimizeni wanawake wote waliojiandikisha washiriki
kupiga kura kwani kura zenu yako ndiyo itakayokupatia kiongozi unayemtaka”,
alisema Mama Kikwete.
Alisema siasa siyo uadui
wala ugomvi bali ni mchakato wa kidemokrasia na kuwataka wagombea wote kunadi
sera zao kwa kufuata utaratibu na amani kwa kuzingatia kanuni na sheria
zilizopangwa na tume ya Taifa ya Uchaguzi ili utulivu na Amani viendelee
kutawala nchini.
Aliwasihi, “Msigombane
kutokana na tofauti ya itikadi za vyama vya siasa, angalieni siasa
zisiwafarakanishe ikafika hatua mkashindwa hata kusaidiana ikiwa ni pamoja na
kushindwa kuzikana kumbukeni nyinyi ni ndugu wa wilaya moja ya Tarime”.
Aidha Mama Kikwete aliwataka
wanawake hao kujenga tabia ya kujiwekea akiba Benki kutokana na fedha
wanazozipata katika kazi wanazozifanya kwa kufanya hivyo wataweza kukopa fedha
nyingi ambazo watafanyia shughuli za maendeleo na hivyo kujikomboa kiuchumi.
“Unganeni pamoja ili muweze kujikwamua kiuchumi,
simameni katika majukwaa teteeni haki zenu, pingeni mila zilizopitwa na wakati
ambazo zinamkandamiza mwanamke na hivyo kumrudisha nyuma kimaendeleo kwa
kufanya hivyo mtaweza kujikomboa kutoka
katika hali ya unyanyasaji”,alisisitiza .
0 comments:
Post a Comment