Home » » KAYA 400 KUKUMBWA NA NJAA TARIME

KAYA 400 KUKUMBWA NA NJAA TARIME

 ZAIDI ya kaya mia nne katika kijiji cha Weigita  kata ya Kibasuka Wilayani Tarime Mkoani Mara huwenda zikakumbwa na njaa kali baada  ya mashamba yao ya mazao zaidi ya hekali elfu tano kupelekwa na maji baada ya Mto Mara kujaa maji na kuhama mkondo wake ambapo maji hayo yamefika hadi mashambani na kwenye makaza ya wananchi huku mifugo 40 ikidaiwa kufa mtoni wakati ikitoka malishoni.
Mwenyekiti wa kijiji cha Weigita amesema kuwa Mafuriko hayo ya maji  Mto Mara  yanadaiwa  kutokea jana majira ya jioni  ambapo ng'mbe 40 kutoka familia 3 zimepelekwa na maji wakati ikivuka mto ikitokea malishoni na kwamba endapo jitihada za haraka hazitafanyika kutatokea maafa makubwa kutokana na Mto kuendelea kumwaga maji.
Pia  zaidi ya vijiji vitano vilivyoko kando kando ya mto mara ambao ulima mazao kando kando mwa Mto mara  mazao yameweza kuharibiwa kutokana na mto mara kujaa na kuhama mkondo ambapo baadhi ya wakazi wa natoka katika vijiji vya Gibaso,Kerende,Murito,Nyarero,Matongo,  .
Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele amewataka wananchi kuacha kulima mazao katika maeneo ambayo si salama ambayo yamekuwa yakitokea mafuriko ya maji ya mara kwa mara nakwamba watu wanapaswa kuhama katika maeneo ambayo si salama  kwa madai kuwa swala la utatuzi wa Mto mara  ni gumu na ni la kitaalamu zaidi na linahitaji pesa nyingi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa