Home » » Halmashauri Wilaya ya Tarime yapata hati safi

Halmashauri Wilaya ya Tarime yapata hati safi

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara imepata hati safi  inayolizisha ambapo taarifa ya fedha imezingatia viwango vya kimataifa vya ukaguzi wa  hesabu za Serikali (ISA) pamoja na taratibu zingine za kiukaguzi.

Akisoma  ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu  za Serikali kuhusu taarifa ya fedha za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa mwaka unaoishia tarehe 30,juni/2012 mbele ya baraza la Madiwani Mkaguzi wa Mkoa wa Mara  Mustafa Mwangaile, alisema kuwa taarifa za fedha zimeakisi kiasi cha kuridhisha mambo yote yaliyohusika.

Mwangaile amesema kuwa hali ya fedha ya Halmashauri  hadi tarehe 30 juni 2012 na matokeo ya utendaji wa mapato halisi kwa mwaka ulioisha,inawiana na viwango  vya kimataifa vya uwaandaaji wa  hesabu za  fedha kwa secta ya umma (IPSAS).

Aidha mkaguzi  huyo ameisisitiza halmashauri  kutumia fedha za ndani  na Ruzuku za serikali kwa wakati  pindi zinapopokelewa kwa madai kuwa kiasi cha 420,484,000 zilihamishiwa kwenye akaunti ya shule mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa madarasa,maabara,ofisi za shule na kituo cha afya Nyakunguru zilikuwa bado hazujatumika hadi kufikia juni 2012.


Hata hivyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Athumani Akalama alisema kuwa fedha hizo kutotumika kwa wakati  mwafaka  ni kutokana na Serikali kuchelewa kuleta fedha ambapo fedha zingine wamekuwa wakizipokea mwisho wa mwaka na hivyo kushindwa kutekeleza miradi kwa wakati.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa