Home » » MKURUGENZI TARIME AZUIA MALIPO FIDIA YA UMEME VIJIJINI

MKURUGENZI TARIME AZUIA MALIPO FIDIA YA UMEME VIJIJINI

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara Athuman Akalama  amezuia malipo ya fedha zilizotolewa na Serikali Kutoka Tanesco kwa ajili ya fidia kwa wananchi walioko katika maeneo yaliyopitiwa na njia ya mradi wa umeme vijijini unaoanzia Mugabiri mpaka  Itiryo baada ya tume aliyoiunda kuchunguza na kuhakiki maeneo  kubaini kasoro  kadhaa zikiwamo za majina hewa 281.

Akiongea na waandishi wa habari  Mkurugenzi Akalama amesema kuwa mwezi mei ,2013 Halmashaauri ilipokea fedha  bilioni 1,541,546,526,.43 Kutoka Serikalini zilizotolewa na Tanesco kwa ajili ya kulipa wananchi nakwamba kutokana na malalamiko ya baadhi ya wananchi ambao maeneo yao yaliyopitiwa na umeme kutoonekana katika orodha ya malipo Mkurugenzi alilazimika kuunda tume ya kuhakiki maeneo kabla ya malipo .

Akama Amesema kuwa Tume imebaini kuwa kuna majina hewa 281 kati ya majina  1,102 yaliyokuwa tayali kwa malipo,pia kuna watu 137 waliofanyiwa uthamini kwenye maeneo yao ambao wana maeneo lakini majina yao hayako kwenye kitabu cha malipo huku wananchi wengine 140 ambao wana maeneo na mali zao na wamepitiwa na mtandao wa umeme lakini hawakufanyiwa uthamini.

Akalama anaongeza kuwa Tume imebaini kuwa  kulikuwa na fomu hewa 132 na jumla ya watu  499 taarifa zao zina  kasoro na zinatakiwa kufanyiwa marekebisho na kwamba watu 430 pekee ndiyo wanatakiwa kulipwa kwakuwa  taarifa zao ni nzuri hazina kasoro jambo ambalo limemladhimu kuzuia malipo   ili kushughulikia malalamiko ya wananchi ili wapate haki zao kwakuwa  kitabu cha malipo kina matatizo na zoezi halikufanyika kwa kufuata maadili akawataka wananchi kuwa wavumilivu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa