WANANCHI wa kijiji cha
Kasahunga wilayani Bunda, mkoani Mara, sasa wanaishi maisha ya wasiwasi, kutokana
na kuibuka kwa kikundi cha watu wasiofahamika, ambao uwaingilia kwenye nyumba
zao nyakati za usiku bila kujua na kufanya uporaji wa vitu mbalimbali na kutaka
kubaka wanawake.
Matukio ya watu kuingiliwa
kwenye nyumba zao bila kujua yametokea usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha
Kasahunga, ambapo kikundi cha watu hao kimeingilia kaya zaidi ya 20 na kufanya
uporaji wa simu za mikononi na pesa tasilimu na kutaka kubaka wanawake.
Watu ambao wameingiliwa na
kikundi hicho wamesema kuwa licha ya kuwa wamefunga milango ya nyumba zao
vizuri, walishitukia mtu mmoja ambaye alikuwa amenyoa upara, akiwa amevaa
bukuta bila shati, akiwa amewaingilia ndani ya vyumba vyao na kutaka kubaka
wananwake.
Aidha, wananchi hao wamesema
kuwa katika miji mingine kikundi hicho kilifungia kwa nje milango ya nyumba za
majirani ili wasitoe msaada na kuingia kwenye nyumba za wananchi hao na kufanya
uporaji wa pesa tasilimu na simu za mkononi na kisha kutokomea kusiko julikana.
Kufuatia hali hiyo wananchi wa
kijiji cha Kasahunga, sasa wanaishi kwa wasiwasi huku wakiyahusisha matukio
hayo na mambo ya ushirikina, lakini baadhi wakidai kuwa pamoja na ushirikina
hicho ni kikundi cha vibaka tu.
Mkuu wa wilaya ya Bunda, Bw.
Joshua Mirumbe, amekemea hali hiyo kwa ni uvunjifu wa amani na ameagiza afisa
tarafa ya Kenkombyo na kamati ya ulinzi na usalama ya kata ya Neruma, pamoja na
uongozi wa kijiji cha Kasahunga kuchukua hatua za haraka kudhibiti hali hiyo
mara moja.
Kijiji cha Kasahunga kimekuwa
na matukio ya ajabu yanayohusishwa na imani za ushirikina, kwani hivi karibuni
wanawake watatu waliuawa na nyumba zao kuchomwa moto, wakituhumiwa kuwa ni
wachawi.
0 comments:
Post a Comment