MALI
za wanachama 17 wa chama cha kuweka na
kukopa cha Vijana Ukerewe Saccos zimeanza
kukamatwa ili kufidia fedha walizokopa sh.
Mil. 14.6 na wakashindwa kuzirejesha.
Meneja
wa chama hicho kilichopo wilaya ya Ukerewe,
Mwanza Bw, Ferdinand Lukansola amewambia wahandishi
wa habari ofisini kwake jana kuwa mali za wanchama hao
zinakamatwa ili kufidia mikopo waliyokopo na kushindwa kurejesha.
Alisema
kabla ya chama hicho kuchukua hatua hiyo suala hilo
lilifikishwa mahakamani na hivi karibun mahakama ilitoa amli
malizi zao zikamatwe ili kufidia madeni yao.
Alifafanua
kuwa baadhi ya mali zao ikiwemo viwanja viwili, thamani
za ndani na mali nyingine kama mifugo vimekamatwa tangu
juzi na baadae zitauzwa ili kufidia mikopo
hiyo.
Ilielezwa
kuwa wadaiwa wengine sugu wapatao 189
wanaodaiwa sh. Mil. 97.8 wamepewa muda na chama hadi septemba
mwaka huu wawe wamerejesha mikopo hiyo vinginevyo
watachukuliwa hatua za kisheria.
Katika
hatua nyingine jeshi la polisi wilayani humo linaendelea na
uchunguzi wa tuuma ya wizi wa sh. Mil. 38.8
zinazowakabili watumishi wawili wa chama hicho cha Vijana
Ukerewe Saccos ili ikithibitika wafikishwe mahakani.
Meneja
wa Chama hicho Feldinand Lukansola alisema
kesi hiyo itafikishwa mahakani wakati wowote kuanzia sasa
baada ya mmoja wa watuumiwa hao aliyekuwa afisa
mikopo wa chama hicho Denis Matundane kukamatwa juzi.
Mtuumiwa
mwingine katika kesi hiyo ni aliyekuwa keshia wa
chama hicho Assa Joseph Makole na kwamba
watumishi hao walipatika na tuuma hizo baada ya kufanyiwa
ukaguzi na ikabainika walitumia udanganyifu na kujipatia fedha
hizo kinyume na taratibu.
Mwenyekiti
wa bodi ya Vijana Ukerewe Saccos Vedastus Toto alisema
wakati akithibitisha taarifa hizi kuwa tatizo hilo
limesababisha chama hicho kishindwe kutoa huduma
nzuri kwa wanachama wake kwa muda mrefu sasa.
Alisema
tatizo hilo lililoanza tangu mwaka 2006 pia limesababisha
chama kishindwe kurejesha kwa wakati mikopo ya tasisi za
kifedha ikiwemo Benki ya CRDB na Self Project .
Hata
hivyo ametumia fursa hiyo kuwataka wanachama wa chama
hicho watambue kuwa hali ya uvumilivu imekwisha
kwa yeyote anayeshindwa kurejesha mkopo kwa wakati na
kuwataka wadaiwa wote watumie muda waliopewa kurejesha mikopo yao
vinginevyo taratibu za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
0 comments:
Post a Comment