KATIKA kijiji cha Nyabisaga kata ya Kyore Wilayani Tarime,
Richard Charles Waitati (14) mwanafunzi wa darasa ka tano katika shule ya
msingi St Jude ambaye ni mkazi wa kijiji cha Nyagisya amefariki dunia
baada ya kujinyonga na kamba ya katani.
Kamanda wa Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Justus
kamugisha amesema kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 6 juni majira ya
saa 12 jioni ambapo chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia ambapo
marehemu aligombania muhindi wa kuchoma na wadogo zake.
Kamugisha anaongeza kuwa baada ya kushindwa kuupata ndipo
alipochukua uamuzi wa kujinyonga nakwamba mwili wa marehemu umefanyiwa
uchunguzi na dactari na kukabidhiwa kwa ndugu zake kwa mazishi.
Wakati huo huo,MKAZI mmoja wa
kijiji cha Genkuru, Matera Marwa Chacha (25) amekutwa akiwa amekufa na
mwili wake kuokotwa katika Kijiji cha Kewanya –Nyamongo Wialayani Tarime akiwa
amepigwa kisogoni na kitu butu na michibuko mgongoni.
Kamanda wa polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Justus Kamugisha
amesema kuwa tukio hilo limetokea juni 6 mwaka huu ambapo chanzo cha
tukio hilo ni marehemu kulisha mifugo yake kwenye chamba la Mwita Mabya (83)
ambaye ni mkazi wa kijiji cha kewanja na kwamba mtuhumiwa amekamatwa yupo kituo
cha polisi Nyamwaga.
Kamugisha amesema kuwa tukio linguine limetokea katika
kijiji cha Gebaso kata ya Nyarukoba Wilayani Tarime ambapo mkazi wa
Gibaso Mkwaya Mwita (48) amejeruhiwa kwa kukatwa na panga kiganja
cha mkono wa kulia na kutenganishwa na mkono huo na mtu aitwae Marwa Ngoka
ambaye alitoroka baada ya tukio hilo.
Kamanda kamugisha amesema kuwa tukio hilo limetoke 6
juni na chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi na kwamba majeruhi amelazwa
katika kituo cha afya Masanga na hali yake inaendelea vizuri.
0 comments:
Post a Comment