Home » » Viongozi wa siasa wajihusisha na uvuvi haramu Bunda

Viongozi wa siasa wajihusisha na uvuvi haramu Bunda



SERIKALI wilayani Bunda mkoani Mara, imewaonywa viongozi wa kisiasa pamoja na watumishi wote wa seriakali, ambao wanajihusisha ama kufadhili uvuvi haramu, kwamba wakibainika hatua kali dhidi yao zitachukuliwa.

Mkuu wa wilaya ya Bunda, Bw. Joshua Mirumbe, ametoa onyo hilo jana, wakati akizungumza na Radio Free Africa, baada ya kuulizwa maswali kwamba ni kwa nini uvuvi haramu katika wilaya ya Bunda, bado uneshamiri sana.

Akijibu maswali hali hayo mkuu wa wilaya ya Bunda, amesema kuwa ni kweli pamoja na jitihada zake  za kusimamia zoezi hilo la kukomesha uvuvi haramu, bado uvuvi huo unaendelea kuwepo wilayani humo.

Bw. Mirumbe amesema kuwa kuna taarifa kwamba baadhi ya viongozi wa kisiasa na watumishi wa umma wanajihusisha na uvuvi haramu.

Kutokana na kuwepo kwa hali hiyo mkuu wa wilaya ya Bunda, ameonya kuwa iwapo kiongozi au mtumishi yeyote, akibainika atawajibishwa ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu na za kisheia.

Amesema kuwa katika jimbo la Mwibara uvuvi haramu hasa umeshamiri katika kijiji cha Kasahunga, ambako kunadaiwa kuna kuna mvuvi mmoja haramu ambaye ni sugu, anayetuhumiwa kuhamasisha wavuvi wengine wa vijiji vya Bunere, Nyansimo, Busambara, Mahyoro, Kasuguti, Mwiseni, Nambuni, Kisorya, Bwanza na Sunsi.


Wananchi wa maeneo hayo wamesema kuwa katika vijiji hivyo wavuvi haramu wanatumia zana zisizo takiwa yakiwemo makokolo na kwamba wanapotakiwa na serikali kusalimisha zana hizo uleta vipande tu, huku makokolo halisi wakiyaacha.

Wananchi hao wamesema kuwa uvuvi haramu hauwezi kuisha kwani baadhi ya viongozi wakiwemo wa vikundi vya ulinzi wa rasilimali za ziwa Victoria (BMU), pamoja na polisi, watendaji wa vijiji na kata, wamekuwa wakifadhili uvuvi huo kwa kupewa mgao kila wiki.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa