JESHI la polisi katika kanda
maalumu ya Tarime na Rorya wamefanikiwa kugundua mashamba mawili ya bangi na
kuyafyeka na kisha mmea huo kuuteketeza kwa moto.
Kamanda wa polisi katika mkoa
wa kipolisi wa Tarime na Rorya, Bw. Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo
limetokea juzi katika kitongoji cha Bumera kijiji cha Kwisarara wilayani
Tarime.
Amesema kuwa polisi wakiwa
katika msako wa kusaka wahalifu waligundua mashamba mawili ya bangi yenye
ukubwa wa ekari tatu na nusu na kwamba kama bangi hiyo ingevunwa ingekuwa na
uzito wa kilo 8,200.
Amesema kuwa mashamba hayo ni
mali ya mwanamke mmoja Bhoke Mwita na mwanaume mmoja Mang’era Wambura, ambao
wote ni wakazi wa wilayani Tarime, na kwamba wote wametoroka na wanatafutwa na
polisi.
Aidha amesema kuwa baada ya
kugundua mashamba hayo, polisi waliyafyeka na kuiteketeza kwa moto bangi hiyo
na kwamba sasa wanawasaka watuhumiwa ili wawafikishe kwenye sheria.
0 comments:
Post a Comment