Home » » Tanapa yatoa msaada wa mabati Tarime

Tanapa yatoa msaada wa mabati Tarime

SHIRIKA  la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia hifadhi ya wanyama Serengeti imetoa msaada wa mabati elfu sita  Wilayani Tarime  kama sehemu yao ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika Wilaya na vijiji vinazopakana na Hifadhi za Taifa.  

Akikabidhi mabati  hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa Mjini Tarime,Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Allan Kijazi amesema kuwa shirika la Tanapa limetoa mabati Elfu 6,000 yenye thamani ya  milioni 124  kwa ajili ya kusaidia katika maendeleo ya wananchi wa Tarime.

Kijazi amesema kuwa mabati hayo  yatasaidia kuezeka madarasa ya shule,nyumba za walimu na vituo vya polisi  na Zahanati ndani ya Wilaya ya Tarime nakwamba msaada huo unatokana na ushirikiano na mahusiano mazuri kati ya Tanapa  na Wilaya ya Tarime.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa  amezitaka Wilaya zingine kuwa wabunifu kama Tarime kwa kuomba  wadau mbalimbali ili wawasaidie katika shughuli za kimaendeleo ambapo pia amewapongeza Tanapa kwa msaada waliotoa kwa  ajili ya maendeleo ya wananchi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa