Home » » Kinana ampa DC wiki mbili

Kinana ampa DC wiki mbili

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amempa muda wa wiki mbili Mkuu wa Wilaya (DC) ya Tarime mkoani Mara, John Henjewele, kuonana na kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Barrick North Mara kupata majibu ya madai kwamba imeacha kutoa asilimia moja ya mapato yatokanayo na uzalishaji wa dhahabu.
Malipo hayo ni kwa ajili ya ada kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, na kuna taarifa kwamba mkataba wa fedha hiyo ulikwisha, wakati uliopo unaitaka kampuni hiyo kutoa kila mwaka hadi mwisho wa uhai wa mgodi huo.
Kinana alifikia hatua hiyo, baada ya kusomewa risala iliyoandaliwa na viongozi wa CCM kata za vijiji saba vilivyoingia mkataba huo.
Katika mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya stendi vya Nyangoto, Kinana alisema ametoa muda huo ili mkuu huyo wa wilaya ahakikishe anapatiwa majibu sahihi na kampuni hiyo.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele ameitaka Barrick kuhakikisha wanajenga barabara ya kiwango cha lami kutoka Tarime hadi mpakani mwa wilaya hiyo na Serengeti katika kijiji cha Murito, kutekeleza makubaliano yaliyowekwa na vijiji vya mgodi huo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa