Home » » Bulaya amwaga misaada Bunda

Bulaya amwaga misaada Bunda

MBUNGE wa Viti Maalumu, kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Mara, Ester Bulaya, ametoa msaada wa mabati kwa ajili ya Kituo cha Polisi Bunda na kikundi cha kwaya cha The Disciples of Christ kilichopata sh milioni moja.
Msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa hivi karibuni.
Akikabidhi msaada huo, mwakilishi wa mbunge huyo, Joash Kunaga, alisema walipewa pesa hizo na mabati na mbunge huyo ambaye kwa sasa yuko jijini Dar es Salaam kikazi ili waviwasilishe kwa wahusika.
Mlezi wa kwaya hiyo, Beatrice Kuyenga, alimpongeza Bulaya kwa kutimiza ahadi yake na kwamba pesa walizopata, watazitumia kurekodi nyimbo mpya za kwaya hiyo.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Balili, Ernest Nkonoki, alisema  kitendo alichoonesha mbunge huyo ni cha busara kwani ni viongozi wachache wanaotimiza ahadi zao kwa wapiga kura.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Bunda, ASP Mayunga Raphael, ambaye alipokea mabati hayo yenye thamani ya sh 500,000, alisema yatatumika kwa kazi iliyokusudiwa.
Alisema msaada wa mbunge huyo kwa Polisi unaonesha namna anavyothamini uwajibikaji wa Jeshi la Polisi wilayani hapo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa