Home » » NORTH MARA WALIPA FEDHA ZA FIDIA KWA WANANCHI WANAOISHI JIRANI NA MGODI WA NYAMONGO

NORTH MARA WALIPA FEDHA ZA FIDIA KWA WANANCHI WANAOISHI JIRANI NA MGODI WA NYAMONGO

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tarime imepokea sh.Bilion 8,012,476,466.26 kutoka  Mgodi wa North Mara Barrick kwa ajili ya kuwalipa fidia kwa awamu mbili wananchi  waliofanyiwa uthamini ili kupisha maeneo kwa ajili ya shughuli za mgodi ambapo watu 382 watalipwa,na malipo hayo yatafanyika wakati wowote baada ya kukamilika taratibu za malipo.

Hayo yameelezwa mbele ya waandishi wa habari na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambaye pia ni Diwani wa kata ya Sirari (ccm) Amosi sagara  nakwamba malipo hayo yatalipwa kwa  wananchi wa Vitongoji vya Gonsara, Nyabigena  na Nyamichare .


Sagara  amesema kuwa malipo hayo ya fidia yamekuja kufuatia malalamiko ya wananchi ya muda mrefu ya kuutaka mgodi wa Nyamongo kuwahamisha wananchi waishio jirani na mgodi ili kuondoa migogoro kadha wa kadha  kati ya wananchi na mgodi.

Sagara ameongeza kuwa kutokana na malalamiko hayo Serikali kupitia Wizara ya ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi ilituma kikosi kazi  kushughulikia matatizo ya uthamini na fidia katika  maeneo yanayozunguka mgodi wa North Mara ili kujenga mahusiano mema  kati ya wananchi na Mgodi.


Aidha Sagara amesema kuwa  kati ya fedha hizo sh. Bilion 5,647,225,356. Zinatarajiwa kulipwa kwa awamu ya 26 na sh.2,365,251,110.26 zinatarajia kulipwa kwa awamu ya 33 na malipo yatafanyika kwanzia hivi sasa.

Mwenyekiti ameeleza kuwa halmashauri  pia imeweza kuwalipa  watu wa kitongoji cha  Nyamichare awamu ya 29 kwa watu 120 jumla ya milioni 477,362,316. Na watu wote wamelipwa na wamechukua malipo yao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa