Home » » MENEJA TRA MARA ASHAURI VIWANDA VIJENGWE.

MENEJA TRA MARA ASHAURI VIWANDA VIJENGWE.

MENEJA Forodha wa Mkoa wa Mara Ben Usaje amesema kuwa Tanzania  haitanufaika na jumuia ya Afrika Mashariki iwapo haitazalisha  viwanda ambavyo vingetengeneza bidhaa kutokana na mali zilizopo na Mataifa yakafika kununua bidhaa hizo zilizotengenezwa Tanzania ili kuongeza pato la nchi.

Meneja huyo amesema kuwa Wafanyabiashara wa nchi ya Kenya wamekuwa wakinunua zao la Ufuta na alizeti kutoka Tanzania na kwenda kutengeneza mafuta katika viwanda vilivyoko nchini kwao kisha mafuta hayo uyauza Tanzania  bila hata kulipa kodi na wakati mazao yametoka Tanzania.

Usaje ameyasema hayo hivi karibuni  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mbele ya Waziri wa Afrijka Mashariki Samwel Sita wakati wa Ziara yake Tarime ambapo waziri huyo aliweza kuzungumza na wananchi juu ya maswala mbalimbali  kuhusiana na soko la  jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hata hivyo Waziri wa Afrika Mashariki Samweli Sita aliwataka wananchi kutokuwa na mawazo finyu katika jumuiya ya Afrika Mashariki hivyo akawashauri wawe na mawazo mapana kwani kujiunga na jumuiya hiyo kunamanufaa makubwa kwa watanzania ambapo hatahivyo majibu yake yalidaiwa kuwa ni ya kisiasa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa