Home » » ATHARI ZA MVUA ZAZIDI KUPAMBA MOTO MKOANI MARA

ATHARI ZA MVUA ZAZIDI KUPAMBA MOTO MKOANI MARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mvua zinazoendelea kunyesha katika Mikoa mbalimbali hapa Nchini zinazidi kusababuisha athari ikiwa ni pamoja na uharibifu wa Mazao, kubomolewa  kwa Nyumba suala ambalo linazidi kuwapa Watanzania changamoto.

Katika wilaya ya Rorya Mkoani Mara katiya kata Tano ambazo ni Bukura, Ikoma,Nyahongo,Nyamagaro,na Korio(Utegi) zimekumba na  Maafa makubwa ambayo yamesababishwa na Mvua zinazoendelea kunyesha nyumba 297 zikiwemo za bati160 na Nyasi137 zimekumbwa na maafa hayo katika kata hizo.

Katika Taasisi za Serikali Jengo moja sekondari ya Nyanduga bweni la wavulanalimeezuliwa bati na shule mbili ya Msingi,Ofisi moja ya Ofisa Mtendaji wa kata ikiwa ni pamoja na Chuo cha Uvuvi kilichopo Shirati Nyancha Taarafa ya Nyamigaro kimetolewa paa katika jengo la kujivunzia jinsi ya kubamba ngozi pamoja na kituo cha Afya Utegi jengo moja limeweza kutikiswa na Upepo huo.

Aidha katika kutoa taarifa Mkuu wa Wilaya ya Rorya Bw: Elias Goroi amesema kuwa baada ya Kuzunguka na kamati ya Maafa Wilaya wamebaini  kuwa Wananchi  wanamahitaji ya Chakula kwani Ekali 910za mazao mbalimbali kama vile Mtama , Mahindi na Migomba zilweza kuhalibiwa na Mvua ya Mawe iliyonyesha ususani katika kata ya Ikoma.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya huyo amesema kuwa Kamati ya Maafa imeona kuwa  kuna Mahitaji ya Chakula Tani 12 Tani 2 za Mtama na Tani 2 za Mahindi ambapo zitasaidia kulisha Watu kwa Mda mfupi

Sanjari na hayo mkuu wa Wilaya ameongeza kuwa amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  aweze kusambaza Madawa  katika Vijiji vilivyoathilika  kwa ajili ya Taadhali ya Milipuko ya Magonjwa ambaya yanaweza kulipuka uku ikiwa zikigawiwa Chandarua 120 kwa akina Mama wajawazito na watoto

Mwisho mkuu wa Wilaya huyo ametoa Mwito kwa jamii kuwa Waweze kujenga Nyumba imara kwa  lengo la kulinda Usalama wao uku akisema katika Tathimini iliyofanywa  hakuna Vifo vilivyotokea kulingana na maafa hayo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa