Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imeipatia
Wilaya ya Bunda jumla ya walimu wapya 223, wakiwemo wa sekondari 137 na
shule za msingi 86.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Simon Mayeye,
alieleza hayo jana wakati wa hafla ya kupokea msaada wa vifaa vya
kompyuta vilivyotolewa na Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma
(PSPF).
Vifaa hivyo vyenye thamani ya sh milioni 5.2, vimetolewa na PSPF kwa
halmashauri hiyo baada ya kompyuta iliyokuwepo kwa ajili ya kuingiza
majina ya watumishi wa halmashauri kupigwa na radi na kuungua.
Mayeye alisema walimu hao wameajiriwa na serikali katika ajira mpya
na kwamba tayari wamekwishaanza kupokewa katika halmashauri yake.
Alisema hadi jana walikuwa wamepokewa walimu 48 wa sekondari na 36 wa
shule za msingi na kuingizwa kwenye kumbukumbu za halmashauri hiyo,
ikiwa ni pamoja na kuanza zoezi la kuwagawa kwenye vituo vyao vya kazi.
Aidha, alisema wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu,
kutokana na idadi kubwa ya walimu kustaafu kwa mujibu wa sheria.
Akikabidhi msaada huo, Ofisa Mfawidhi wa PSPF mkoani Mara, Sudi
Hamza, alisema wametoa vifaa hivyo baada ya halmashauri hiyo kupeleka
maombi kutokana na kompyuta iliyokuwepo kupigwa na radi.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment