Home » » MAHABUSU APANDA JUU YA MTI APIGA YOWE KUCHELEWA KWA KESI.

MAHABUSU APANDA JUU YA MTI APIGA YOWE KUCHELEWA KWA KESI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MAHABUSU katika Gereza la Wilaya ya Tarime Mkoani Mara  leo asubuhi ameonekana akiwa juu ya Mti  ulio ndani ya  gereza akipiga yowe na kuomba wanaharakati,Waandishi wa habari na Haki za Binadamu wamsaidie baada ya kuchelewa kwa kesi yake inayomkabili ya mauwaji ya mwaka 2010.

Mahabusu huyo akisikika kwa sauti alilalamika kuwa tangu akamatwe mwaka 2010 kwa kukabiliwa na kesi ya mauwaji hadi sasa kesi yake inaendelea kupigwa chenga bila kushughulikiwa na kuzidi kusota gerezani.

Mahabusu huyo  alipiga yowe akiwataka wanaharakati,Haki za Binadamu na akawaomba waandishi wa habari waandike malalamiko yake huwenda Serikali itamsaidia ili kesi yake ikamilike kwa madai kuwa kesi yake inapigwa tarehe  na amechoka kuishi gerezani bila matumaini ya hatima ya kesi yake.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele  alisema kuwa amepokea taarifa ya mahabusu huyo kulalamika juu ya mti juu ya kucheleweshwa kwa kesi yake na kuahidi kufatilia kwakuwa  yuko kikazi Kata ya Nyamwaga Wilayani Tarime.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa