Home » » MIAKA 30 JELA KWA UNYANG'ANYI

MIAKA 30 JELA KWA UNYANG'ANYI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MAHAKAMA ya Wilaya ya Musoma, mkoani Mara, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela pamoja na kuchapwa viboko 10, mkazi wa Mtakuja, Makarani Wambura (25) baada ya kupatikana na hatia ya unyang’anyi wa kutumia silaha.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Karim Mushi, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka.
Hakimu Mushi, alisema ameridhika pasipokuacha shaka  na ushahidi huo, hivyo kumhukumu Wambura kifungo cha miaka 30 jela, pamoja na kuchapwa viboko 10 wakati akiingia gerezani.
Awali, Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Jonas Kaijage,  alidai Septemba 29 mwaka jana, saa 6 usiku, katika baa ya Simba Club, iliyoko katika Mtaa wa Mtakuja mjini Musoma,  mshitakiwa akiwa na wenzake watano ambao walitoroka, walivamia baa hiyo na kufanikiwa kuiba pesa taslimu sh 350,000 na vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh 900,000, mali ya Martha Gikaro, mkazi wa mtaa huo.
Alidai kabla ya kufanya unyang’anyi, walitumia silaha mbalimbali za jadi yakiwemo mapanga na marungu ili kufanikisha kitendo hicho.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa