Home » » WANANCHI WAHIMIZWA DAFTARI LA WAPIGA KURA

WANANCHI WAHIMIZWA DAFTARI LA WAPIGA KURA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WANANCHI wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara, wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la kupiga kura ili uchaguzi utakapofika waweze kupata haki yao ya msingi ya  kuwachagua viongozi wanaowataka.
Kauli hiyo imetolewa na mjumbe wa Kamati Tendaji ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Butiama, Yusufu Kazi, wakati akiwashukuru wajumbe kwa kumuamini na kumpa kura nyingi kwenye uchaguzi wa mkutano mkuu wa Jimbo uliofanyika hivi karibuni.
Kazi, alisema wananchi wote wanatakiwa kwenda kujiandikisha kwenye daftari hilo zoezi litakapoanza, kwani bila kujiandikisha watakosa haki yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wanaowataka kwa ajili ya maendeleo yao.
Pamoja na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari hilo, alitoa shukrani kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kuwapa Wilaya Butiama.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa