Home » » MAOFISA KILIMO LAWAMANI.

MAOFISA KILIMO LAWAMANI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAKULIMA wa mahindi wilayani Tarime katika mkoa wa Mara, wameuomba uongozi wa wilaya hiyo kusaidia kuwadhibiti watumishi wakiwamo maofisa wa Kilimo katika tarafa ya Inchugu, ambao wamekuwa kero kwa kuwakamata wakiwa na mazao yao wanapokwenda kuyauza katika masoko ya ndani na nje ya wilaya hiyo.
Akizungumza na gazeti hili, Diwani wa Kata ya Pemba, Serenga Wangwe alisema kwa sasa wilayani hapa kuna mavuno ya mazao yakiwemo mahindi, na wakulima wakitaka kwenda kuyauza mjini Tarime ama nje ya wilaya hiyo wamekuwa wakisumbuliwa kwa kukamatwa na baadhi ya watumishi wa Serikali wakiwemo wa Idara ya Kilimo Kituo cha Sirari huku watumishi hao wakioneshwa vielelezo na barua za kutoka vijijini.
Alisema hali hiyo inawafanya wakulima kushindwa kwenda kuuza mazao yao kwa bei ambayo ingewainua na kuyauza kwa walanguzi kwa kupewa bei ya chini kwa gunia moja la kilo 108 kwa Sh 50,000, huku walanguzi nao wanaodai wana vibali vya kusafirisha mahindi, wanakwenda kuyauza wilayani Sh 56,000.
 CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa